Changamoto sita za kimazingira Zanzibar, wadau wapendekeza hatua za kuchukua

Changamoto sita za kimazingira Zanzibar, wadau wapendekeza hatua za kuchukua

Zanzibar. Zanzibar inakabiliwa na changamoto za kimazingira, ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa kina cha bahari, uvamizi wa maji ya chumvi, mmomonyoko wa fukwe, na hali mbaya ya hewa.

Ofisa Uratibu wa Wizara ya Uchumi wa Buluu, Omar Mohamed, ameeleza changamoto hizo Machi 10, 2025 wakati wa warsha kuhusu uchumi rejelezi (Circular Economy) na Uchumi wa Buluu iliyoandaliwa na Afrika 21 kwa kutanisha waandishi wa habari, wataalamu wa uchumi relejezi na uchumi wa buluu kutoka Afrika, hususan mataifa ya pwani na visiwa vya Bahari ya Hindi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Hamad Bakar Hamad akizungumza na waandishi wa habari

Omar Mohamed amebainisha kuwa uharibifu wa miamba ya matumbawe unatishia sekta za uvuvi na utalii, huku uvamizi wa maji ya chumvi na mabadiliko yasiyotabirika ya mvua yakihatarisha kilimo na vyanzo vya maji safi.

“Tunahitaji kuchukua hatua sasa ili kulinda maisha na usalama wa chakula,” amesema akiongeza miongoni mwa madhara ni jamii za pwani zikilazimiaka kuhama kwa lazima kutokana na kupungua kwa ardhi.

Amesema asilimia 23 hadi 54 ya watu wanakabiliwa na tatizo hili. Aidha, kupungua kwa idadi ya samaki kumeathiri ustawi wa wavuvi, hivyo kuhatarisha riziki na usalama wa chakula.

Akifafanua zaidi, amesema, “tafiti na shuhuda za wavuvi zinaonyesha kupungua kwa mazalia ya samaki, hali inayolazimisha Serikali kuchukua hatua madhubuti za kuimarisha sekta ya uvuvi.”

Umuhimu wa uhifadhi wa mazingira

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Hamad Bakar Hamad, amesisitiza kuwa uchumi wa Zanzibar unategemea sana bahari, huku sekta za uvuvi na utalii zikiwa nguzo kuu za maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

 “Sekta hizi zinategemewa na takriban theluthi mbili ya wakazi wa Zanzibar, huku uvuvi ukichangia kati ya asilimia nne hadi 8 ya Pato la Taifa (GDP) na utalii ukichangia zaidi ya asilimia 29,” amesema Hamad.

Tasnia nyingine muhimu ni pamoja na ufugaji wa baharini, kilimo cha mwani, na uvunaji wa holothuria (sea cucumbers), ambavyo vina mchango mkubwa katika uchumi wa Zanzibar.

Mwaka 2024, uzalishaji wa mwani ulifikia takriban tani 18,000, huku asilimia 99 ya biashara za kimataifa zikitegemea rasilimali za bahari.

Licha ya mchango huu wa kiuchumi, Hamad amekiri kuwa Zanzibar inakabiliwa na changamoto za uendelevu, akihimiza mabadiliko ya mbinu za matumizi ya rasilimali ili kuhakikisha manufaa ya muda mrefu kwa mazingira na jamii.

Hatua zinazochukuliwa

Katibu Mkuu Hamad amesema Serikali inawahamasisha wanawake wanaojihusisha na kilimo cha mwani pamoja na wavuvi kuhamia maeneo ya kina kirefu cha bahari ili kulinda akiba ya samaki na kuongeza mavuno.

 “Ili kuwezesha mabadiliko haya, Serikali imewapatia wavuvi na wakulima wa mwani zaidi ya boti 1,000 kwa riba ya asilimia 0,” amesema.

 Aidha, amebainisha wanafanya jitihada kutafuta masoko bora na kuanzisha viwanda vya usindikaji ili kuimarisha mnyororo wa thamani wa bidhaa zinazozalishwa.

“Mkakati wetu unahakikisha kuwa wanawake hawaachwi nyuma katika shughuli zao za kiuchumi, bali wanapewa nyenzo na fursa za kustawi katika Uchumi wa Buluu. Wizara yetu imejizatiti kuwasaidia wanawake kuendelea kushiriki kikamilifu katika sekta hii,” amefafanua.

 Amesisitiza kuwa dhamira ya Serikali katika uhifadhi wa mazingira na uwezeshaji wa kiuchumi inalenga kuhakikisha kuwa rasilimali za bahari za Zanzibar zinaendelea kunufaisha jamii huku zikihifadhiwa kwa vizazi vijavyo.

Ili kukabiliana na changamoto hizi, Omar Mohamed amependekeza kupanua uchumi wa buluu kupitia kilimo cha mwani na bioteknolojia ya baharini, kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala, na kutekeleza miradi ya kulinda fukwe.

Pia amesisitiza umuhimu wa utalii endelevu na kuwawezesha vijana kwa ujuzi wa uhifadhi wa mazingira na mbinu za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal

Ruling party Chama Cha Mapinduzi-Zanzibar has said it is ready to task state organs to investigate some of the claims against its government that have been raised by opposition politicians on the Abeid Amani Karume International Airport (AAKIA).Continue Reading