CCM yaahidi ilani itakayotatua changamoto za ajira kwa vijana

CCM yaahidi ilani itakayotatua changamoto za ajira kwa vijana

CCM yaahidi ilani itakayotatua changamoto za ajira kwa vijana

Bukoba. Katika kukabiliana na uhaba wa ajira Tanzania, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) -Bara, Stephen Wasira amesema chama hicho kitakuja na ilani bunifu kwenye uchaguzi mkuu 2025 ili kuongeza kasi ya mapato kwa wananchi wote ikiwemo vijana kufanikiwa kiuchumi.

Amesema ilani hiyo itasaidia kukabiliana na changamoto ya uchache wa ajira na lawama kubwa zinazotolewa kwa Serikali inayoundwa chama hicho kutoka kwa vijana wanaohitimu vyuo mbalimbali nchini na nje ya nchi.

Wasira anatoa kauli hiyo katika kipindi ambacho baadhi ya makundi yameanza kujitokeza hadharani ikiwemo walimu wasio na ajira nchini, kufanya mikutano na vyombo vya habari kuishinikiza Serikali kuwapa ajira.

Akizungumza leo Machi 22, 2025 kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Kemondo, Tarafa ya Katerero Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, Wasira amesema kilio cha ajira wanakisia lakini Watanzania na vijana wanapaswa kufahamu chama hicho kimefanya makubwa na maendeleo yanavyokuja yanakuwa na changamoto zake.

Amesema pamoja na changamoto mpya kama kuwa na wasomi wengi, chama hicho ni lazima kije na mkakati wa kuwalinda hasa vijana kutokana na umuhimu wao.

“Tumeshakubalina tutakuja na ilani bunifu katika uchaguzi mkuu wa 2025 itakayotoa upendeleo maalumu kwa vijana, kuja kuongeza kasi ya mapato kwa vijana ili waweze kufanikiwa kiuchumi,” amesema.

Wasira amesema hawawezi kulitenga kundi hilo kwa kuwa ni kubwa na lina ushawishi mkubwa, hivyo wanalitegemea katika kuleta mageuzi ya kiuchumi Tanzania.

“Katika kamati ya kutengeneza ilani, mimi mwenyewe ni mjumbe, ninachosema nina uhakika nacho, lazima tuje na ilani bunifu kukabiliana na tatizo la ajira, vijana wanahitaji kumiliki uchumi,” amesema nakuongeza:

“Tumekubaliana lazima vijana wapewe nafasi maalumu kama wanafanya kazi ya uvuvi, lazima wafanye shughuli hiyo kisasa, lazima tuwasaidie zana za kazi za kisasa,” amesema.

Wasira amesema kulingana na mazingira ya sasa, wamefanya tathmini na kutambua vijana hawahitaji fedha za kusubiria kwa muda mrefu na badala yake wanataka fedha za haraka haraka.

“Ndiyo ujana huo wala huwezi kuwalaumu kwa sababu tumewasomesha halafu tumewapa simu za kupangusa na kidole, dunia nzima iko kiganjani mwao na wanafuatilia yanayojiri duniani,” amesema.

Amesema chama hicho kimetafakari kuna miradi wakileta itakuja kunufaisha vijana ikiwemo kufanya uvuvi wa kisasa kwa kuwapatia vifaa vinavyokidhi mahitaji hayo.

“Kama unafanya kilimo, basi tunaangalia mazao ya muda mfupi, wanalima na kuvuna kama bustani za nyanya wanalima na kuvuna wanauza na kununua vocha, maana vijana wapo tayari kulala njaa ili mradi tu wapate vocha,” amesema.

Katika hatua nyingine, mbunge wa Bukoba Vijijini, Jasson Rwekiza amesema katika kipindi cha miaka minne Serikali imefanya vizuri hasa kwenye sekta ya maji, walipokea fedha ya utekelezwaji miradi 38 ikiwemo Lukindo, Katare na Lubale.

“Miradi mingi imekamilika na baadhi imeanza kufanya kazi, maeneo mengi yataanza kunufaika na huduma ya maji safi na salama, jumla ya miradi yote ni zaidi ya Sh25 bilioni,” amesema.

Katika sekta ya elimu, Sh29.6 bilioni wamejenga madarasa 194, matundu ya vyoo 195 na shule zingine ili kuwarahisishia wanafunzi kusoma mazingira mazuri na rafiki huku katika sekta ya afya Serikali ikiwapa zaidi ya Sh3 bilioni.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Richard Kasesela amesema dhambi kubwa inayowatafuna wanaCCM pale tunapopata madaraka ni kiburi na kujisahau kwa sababu ya madaraka.

“Jambo lingine tamaa, ulafi, jamani madaraka anatoa Mungu, waacheni nao wagombee ili ukishinda nawe ushinde kwa haki bila nongwa,” amesema.

Awali, mjumbe wa halmashauri kuu Taifa kutoka Mkoa wa Mbeya, Ndele Mwaselela amesema kutokana na utekelezwaji wa ilani katika kuleta maendeleo, anaamini uchaguzi ujao wanaenda kushinda kwa kishindo.

“Kazi iliyobaki ni wanaCCM kuwa pamoja kushirikiana na kuzungumza lugha moja kukabiliana na vyama vya upinzani,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading