TCD inavyotoa fursa kwa Chadema, ACT kuunda ushirikiano Uchaguzi Mkuu 2025

Habari ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), si yenye kushtua, maana ni utaratibu wa vyama vyenye wabunge kupishana katika uongozi wa taasisi hiyo.

Habari kuwa Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Dorothy Semu, ndiye amekuwa Makamu Mwenyekiti wa TCD, ndiyo inasogeza mjadala. Mwenyekiti Chadema, Mwenyekiti TCD, halafu Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Makamu Mwenyekiti TCD. Watafanyaje kazi?

Tafsiri ambayo haikwepeki baina ya vyama vya Chadema na ACT-Wazalendo ni kuwa vimekuwa hasimu kwenye jukwaa la “vyama vya upinzani”. Yaani, baada ya mchuano wa CCM na vyama vya upinzani, nje ya chama hicho kinachoongoza dola Tanzania, kuna msigano wa wazi kati ya Chadema na ACT-Wazalendo.

Vyama vya ACT-Wazalendo na Chadema, mara nyingi vina mitazamo ya aina moja kuhusu masuala, lakini hutofautiana njia ya kuyafikia mambo husika. Ajabu, tofauti hiyo ya njia ndiyo husababisha migongano, kiasi cha viongozi na wafuasi wao hulumbana majukwaani na mitandaoni hadi kudhihirisha uhasimu mkubwa uliopo baina yao.

Mathalan, Chadema na ACT-Wazalendo, wote maono yao yanaweza kuwa yanasema Mwanza kuna sangara wa kutosha. Halafu, wakatofautiana jinsi ya kufika Mwanza. Chama kimoja kikasema njia bora ni kwenda kwa treni, kingine kikawa na mapendekezo ya kutumia barabara. Treni na barabara huzua zogo na kusahau makubaliano ya kimsingi kuwa sangara wapo Mwanza.

Huu siyo mfano, bali ndivyo ilivyokuwa. Chadema walijenga msimamo kwamba wanahitaji Katiba mpya. ACT-Wazalendo, wakatoa maono yao ya kupata Tume Huru ya Uchaguzi kuelekea Katiba mpya. Mpaka hapo, utaona kuwa Chadema na ACT-Wazalendo, walikuwa na makubaliano kwamba Katiba mpya ni lazima.

Sasa, Katiba mpya moja kwa moja, ambao ni msimamo wa Chadema, halafu Tume Huru kwanza kuelekea Katiba mpya, mtazamo wa ACT-Wazalendo, ikawa ndiyo hoja ya mapambano baina ya vyama hivyo. Hawatofautiani hatima, wanatofautiana namna ya kuifikia.

Namna ambavyo hutofautiana njia ya kufikia hatima ya jambo, ndivyo hujenga misuguano kijamii. Upo wakati watu hujiuliza, kwani wapinzani wa Chadema ni ACT-Wazalendo au CCM? Swali hilohilo lipo upande wa ACT-Wazalendo dhidi ya Chadema.

Kipindi hiki, Mbowe na Dorothy, wamekabidhiwa uongozi wa TCD, lipo swali linaweza kuwa linagonga vichwa vya wengi; watafanyaje kazi? Watasikilizana na kuelewana kwa sababu wanatambua hatima yao ni moja au watachagua kulumbana kwenye njia ya kufikia hatima kama kawaida yao?

Ushauri kwa Mbowe, Dorothy

Rais wa 16 wa Marekani, Abraham Lincoln anatajwa kuwa bora kuliko wengine 45 waliopata kuongoza taifa hilo kubwa duniani. Sifa zipi ambazo zinampambanua kwa ubora miongoni mwa wengine wote waliowahi kukalia ofisi ya Rais wa Marekani, Oval Office? Kwa utangulizi tu ni kwamba ukiona kiongozi anaitwa bora, ujue alionyesha ubora.

Rais wa 44 wa Marekani, Barack Obama, anatajwa kuwa mmoja wa viongozi bora zaidi kupata kuliongoza Taifa la Marekani. Obama mwenyewe alipata kujipambanua katika hotuba zake kwa kunakili nukuu nyingi za Lincoln, zaidi alishakiri kwamba alijifunza mengi kiuongozi kupitia mtindo wa uongozi wa Lincoln.

Kitabu kinachoitwa “Team of Rivals: The Political Genius of Abraham Lincoln”, kilichoandikwa na mwanahistoria wa Marekani, Doris Kearns Goodwin na kuchapishwa mwaka 2005, kinaeleza kwa nini Lincoln alikuwa bora. Kinadhihirisha kwamba Lincoln ni kiongozi wa kufaa kuigwa na vizazi vyote. Obama amepata kukiri kuwa kitabu hicho kilimsaidia kuteua Baraza la Mawaziri.

Watu wengi humsifu Lincoln kwa uongozi wa utu, ulioweka misingi ya haki za binadamu na kupiga marufuku ubaguzi. Ni Lincoln aliyefanya kampeni ya kupinga biashara ya utumwa Marekani na alipochaguliwa kuwa Rais, alitangaza ukomo wa biashara ya utumwa na kupitisha azimio la kumuweka huru kila mtumwa (Emancipation Proclamation), Januari mosi, 1963.

Hata hivyo, yapo mengi yenye kumfanya Lincoln awe bora. Alionyesha utofauti chanya ndiyo maana viongozi wengi hutamani kumuiga. Ni hakika kwamba kila kiongozi wa nyakati za sasa akimuiga Lincoln na kumpatia, naye atatamkwa kuwa bora. Viongozi aina ya Lincoln hutokea mara chache, ili kutoa tafsiri ya maana ya uongozi uliotukuka.

Ndani ya kitabu cha Team of Rivals, sifa kubwa ya Lincoln inatajwa ni jinsi ambavyo alikuwa na uwezo mkubwa wa kumudu presha za kiuongozi. Uwezo wake mkubwa wa kutambua karama na uwezo wa watu wengine, hata wale waliokuwa wapinzani wake wa kisiasa. Hapa ndipo hasa kwenye ukuu wa Lincoln na ndipo ushauri kwa Mbowe na Dorothy, unapopenya.

Ni sababu ya Goodwin kukiita kitabu chake, Team of Rivals; The Political Genius of Abraham Lincoln, akimaanisha kwamba Serikali ya Lincoln ilijumuisha watu waliokuwa wapinzani wa kisiasa wa Lincoln, lakini mwenyewe alitambua kile walichokuwa nacho, akawaheshimu, akawateua na kushirikiana nao kufanya kazi bora kwa nchi.

Kwa tafsiri ambayo si rasmi, unaweza kusema Timu ya Wapinzani; Maarifa ya Kisiasa ya Abraham Lincoln. Sababu namba moja ambayo ilimfanya Lincoln atambue uwezo wa wapinzani wake na kuwapa nafasi za uongozi ni utulivu na usikivu wake. Alipenda kusikiliza watu wenye mitazamo tofauti na ya kwake, ndiyo maana aliweza kuujua ubora wa wapinzani wake.

Washindani wa Lincoln wa kisiasa ambao aliwapa nafasi kwenye Baraza la Mawaziri ni Waziri wa Fedha, Salmon Chase, Waziri wa Mambo ya Nje, William Seward, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Edward Bates. Hao ni kuwataja kwa uchache, waliopata kutoana jasho la kisiasa na Lincoln, lakini akatambua uwezo wao na kuwateua wamsaidie kazi.

Obama anaposema kitabu cha Team of Rivals kilimjenga katika kufanya uteuzi wa Baraza la Mawaziri, anaaminisha kweli. Maana alishindana vikali na aliyekuwa Seneta wa New York, Hillary Clinton, kuwania tiketi ya chama cha Democratic kuwa mgombea urais katika Uchaguzi wa Rais wa Marekani mwaka 2008. Hata hivyo, Obama baada ya kushinda urais alimteua Hillary kuwa Waziri wa Mambo ya Nje.

Hoja ya kushika

Imeelezwa kuwa Lincoln aliweza kufanya kazi na wasaidizi wake, ambao aliwateua miongoni mwa wapinzani wake kwa kuwa alikuwa msikivu. Kusikilizana ndiyo njia itakayowawezesha Mbowe na Dorothy kufanya kazi kwa maelewano, licha ya historia ya vyama vyao kutofautiana na kulumbana mara kwa mara.

Katika kusikilizana, pengine wakafanya kazi iliyotukuka, ambayo inaweza kushawishi ushirikiano mkubwa mbele ya safari. Tanzania itafanya uchaguzi wa Serikali za mitaa, Novemba 2024, hivyo huu ni mwaka wa uchaguzi. Vyama vya ACT-Wazalendo na Chadema, vitakuwa imara zaidi kwenye uchaguzi, endapo vitashirikiana.

Tanzania itafanya Uchaguzi Mkuu 2025, kwa maana hiyo umebaki mwaka mmoja. Chadema na ACT-Wazalendo, ili kuikabili CCM wakiwa imara, wanahitaji ushirikiano. Hivyo, kitendo cha Mbowe na Dorothy, kuongoza TCD, ni fursa ya kuona jinsi ambavyo inawezekana kufanya kazi pamoja.

Uchaguzi Mkuu 2020, Chadema na ACT-Wazalendo, walikuwa na makubaliano. Walishiriki uchaguzi kama timu. Matokeo yaliwasambaratisha. Walisimama pamoja kuyakataa matokeo. Wakatofautiana jinsi ya kuyaendea matokeo.

Chadema walikataa kila kilichotokana na Uchaguzi Mkuu 2020. ACT-Wazalendo, wao waliyakataa, halafu wakachukua walichopata. Hilo lilizua malumbano baina ya vyama hivyo.

TCD ni taasisi inayounganisha vyama vyenye uwakilishi bungeni; CCM, Chadema, ACT-Wazalendo na CUF, wakati NCCR-Mageuzi ambacho hakina uwakilishi, chenye ni mwanachama mshiriki, maana hadi Uchaguzi Mkuu 2020, kilikuwa na ushiriki bungeni. Kila mwaka unachaguliwa uongo mpya. Mbowe na Dorothy, wataongoza TCD kwa mwaka mmoja.Continue Reading

Mwananchi Credit blocked from selling seized lorries in Sh9.2m row

Mwananchi Credit has failed in its bid to lift a court order blocking the microlender from selling two lorries belonging to two traders, which were seized over a disputed loan.

High Court judge Kizito Magare upheld the injunction issued by a Milimani magistrate blocking the microlender from selling the two lorries — a Mercedes truck and a Scania lorry, which were attached in March 2021.

The court was informed that Peter Kamau Githua and Elizabeth Wanjiku borrowed a loan of Sh2.5 million and charged the lorries as security. The traders said they had repaid Sh3 million but the lender was still demanding more money.

Justice Magare noted that the traders had pleaded and demonstrated that it was likely that the entire debt had been paid.

Secondly, the judge said, Mwananchi Credit is not a mortgagor as the chattel mortgage (the loan used to purchase the vehicles and which served as security of the loan) was not registered, making the attachment void and the amount claimed fictitious.

“There is also a contention that a sum of Sh9,254,767 is outstanding as per the records held by the appellant (Mwananchi). I am not a student in sorcery and magic, but I am unable to fathom the labyrinth or mathematical permutations and flagrant distortion of figures that caused a sum of Sh2,500,000 to become Sh9,254,767.24 despite payment of three million shillings,” the judge said.

The court was informed that the repossession of one of the lorries was made in a gangster-like move.

“If we are to let our microfinance fall into the same school as the shylocks, the court will be missing its duty,” said the judge.

The microlender moved to the High Court after the lower court blocked the sale arguing that there was a valid claim and that it had been registered.

But the traders maintained that they had paid all amounts due.

Ms Wanjiku said in an affidavit that one of the lorries was involved in an accident but they continued paying the loans.

In March 2021, the lender attached one of the vehicles and threw out the driver on the transit claiming a balance of Sh9.2 million.

Senior principal magistrate D.W. Mburu then granted the injunction in October 2021, pending the determination of the case.

Continue Reading

Wapata dawa ya utoro, mimba kwa wanafunzi wa kike

Mufindi. Ili kupunguza utoro na mimba kwa wanafunzi wa kike katika shule ya sekondari Ilongo iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Mufindi, Wakala wa Misitu Tanzania (TFS), kupitia shamba la miti la Sao Hill wametoa vifaa vya ujenzi wa bweni la wasichana vyenye thamani ya zaidi ya Sh30 milioni kwa ajili ya ujenzi wa bweni hilo.

Akizungumza baada ya kupokea vifaa hivyo leo Juni 29, 2024, Ofisa Elimu Sekondari Wilaya Mufindi, Daniel Mapilya amesema msaada huo uliotolewa na Sao Hill, una manufaa katika kupunguza viashiria hatarishi vya mimba kwa watoto wa kike shuleni.

“Wanafunzi hawa walikuwa wanapanga mitaani kwenye nyumba za wananchi bila kuwa na uangalizi wa aina yoyote, hivyo msaada huo wa vifaa vya kujenga bweni kutoka Sao Hill utawasaidia kusoma kwa pamoja wakiwa bwenini bila usumbufu wowote,” amesema Mapilya.

Amesema baada ya kukamilika kwa ujenzi wa bweni hilo, litawasaidia wanafunzi wao kwa kuwapunguzia kutembea umbali mrefu wa zaidi ya kilometa nane hadi kufika shuleni hapo.

Kwa upande wake, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ikweha, Tabia Chibwana amesema uwepo wa bweni hilo utasaidia kupunguza changamoto ya watoto wa kike kupata ujauzito, hivyo litasaidia watoto hao kutimiza ndoto zao.

Ofisa huyo amesema shule hiyo ina zaidi ya wanafunzi 448, kati yao 268 ni wanafunzi wa kike ambapo tangu kuanzishwa kwa shule hiyo mwaka 2007, wamekuwa wakipata changamoto ya wanafunzi hao kurubuniwa, hali ambayo imesababisha kupata ujauzito kwa sababu ya kukaa mitaani kwenye vyumba vya kupanga.

Mhifadhi Mkuu wa Sao Hill, Yebby Yoram amesema wataendelea kusaidia kadri bajeti itakavyokuwa kusaidia miradi kama hiyo katika maeneo mengine.

“Maombi mengi yanahusu miradi kama hii lakini kuna baadhi ya shule tumesaidia miradi hiyo ikiwemo shule ya sekondari Luganga, Changalawe pamoja na shule zingine,” amesema.

Awali akisoma taarifa ya vifaa hivyo, Mhifadhi Mwandamizi wa shamba la Sao Hill, Peter Nyahende amesema Sao Hill wanatambua umuhimu wa mazingira bora ya kutolea elimu kwa watoto hao kwa kukabidhi vifaa hivyo kwa ajili ya ujenzi wa bweni la wasichana katika shule hiyo.Continue Reading

Pingamizi mgombea ADC lapuuzwa, wanachama 197 kuamua

Dar es Salaam. Wakati wapiga kura 197 wakitarajia kufanya uamuzi wa kikatiba kumchagua mwenyekiti mpya wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Kamati ya uchaguzi huo imesema pingamizi alilowekewa mmoja wa wagombea wa nafasi ya mwenyekiti, Shabani Haji Itutu halijafuata kanuni za chama.

Itutu aliwekewa pingamizi na wanachama saba wa ADC, Ibrahim Pogora, Asha Milongea, Asha Mzee, Khadija Tambwe, Maisala Khamis, Doni Mnyamani na Halima Msumali wakidai ni mwanachama wa chama kingine cha upinzani.

Katibu wa kamati ya uchaguzi, Innocent Siriwa ameiambia Mwananchi Digital leo Ijumaa, Juni 28, 2024 kwamba wamepokea pingamizi hilo, lakini kwa mujibu wa kanuni za chama, kamati haitalifanyia kazi.

“Kwanza limekuja nje ya muda wa mapingamizi uliowekwa, lakini pia kanuni za chama zinaelekeza mtu anayetakiwa kumwekea pingamizi mgombea ni mgombea mwingine, sio wanachama,” amesema Siriwa.

Akizungumzia mchakato wa uchaguzi huo utakaofanyika kesho Jumamosi, Siriwa amesema mkutano mkuu utaanza saa 2:00 asubuhi na wanatarajia mchakato wote hadi kupata viongozi wapya wa ADC kukamilika saa 10:30 jioni kwenye hoteli ya Lamada, Ilala jijini Dar es Salaam.

“Wapiga kura ni 197 kutoka Bara na Zanzibar, wataanza kwa kumchagua mwenyekiti (nafasi hiyo inawaniwa na Itutu aliyewahi kuwa makamu mwenyekiti na Doyo Hassan Doyo aliyewahi kuwa katibu mkuu), mshindi atakabidhiwa madaraka na mwenyekiti anayemaliza muda wake (Hamad Rashid).

“Atakapokabidhiwa, mwenyekiti mpya ndiye ataendelea na mchakato wa kuwapata makamu mwenyekiti wa Bara na Zanzibar,” amesema Siriwa.

Wanaowania nafasi hiyo upande wa Bara ni Scola Kahana na Hassan Mvungi na Zanzibar ni Fatma Salehe na Shara Amrani huku pia kesho utafanyika uchaguzi wa nafasi 19 za wajumbe Bodi ya uongozi taifa.

Kwa mujibu wa Siriwa, nafasi hizi wagombea wake watachukua na kurudisha fomu siku hiyohiyo ya uchaguzi (kesho), watapigiwa kura siku hiyo ukumbini na kati ya watakaochaguliwa, robo au nusu ya idadi hiyo wanapaswa kutoka Zanzibar.

Kabla ya uchaguzi huo kesho, leo Ijumaa kuanzia saa moja usiku, Bodi ya Taifa ya uongozi ya ADC itakuwa na mkutano mkuu maalumu kupitisha ajenda za mkutano huo mkuu wa uchaguzi.

“Mkutano mkuu unatambuliwa na Bodi ya taifa ya uongozi, ambayo ndiyo itapitisha ajenda za mkutano mkuu wa kesho,” amesema Siriwa.

Kampeni za uchaguzi wa chama hicho zitakoma leo saa 12 jioni ambapo zitafungwa tayari kwa uchaguzi huo kesho, huku wagombea wakisisitizwa kufuata kanuni na taratibu za chama ambazo zimeelekeza kufanya kampeni za kukijenga na kugusa maisha ya wananchi.Continue Reading

Kariakoo ngoma mbichi

Licha ya Serikali kutangaza kuwa itafanyia kazi malalamiko ya wafanyabiashara wa Kariakoo, ikiwemo kusitisha kamatakamata iliyokuwa ikifanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), baadhi ya wafanyabiashara wamesema Rais Samia Suluhu Hassan ndiye anapaswa kutoa tangazo hilo..Continue Reading