Bunge latunga kanuni ngumu kwa wanahabari, wadau wang’aka

Dodoma. Bunge la Tanzania limetunga Kanuni mpya za mwaka 2023, ambazo zimeweka adhabu kwa waandishi wa habari na masharti ya namna ya kupiga picha ndani ya ukumbi wa Bunge.

Kanuni hizo ambazo zimechapishwa katika Gazeti la Serikali (GN) ya Machi 21, 2023 zimeeleza maeneo yanayoruhusiwa kupiga picha na kamera zitakazotumika zitalazimika kuruhusiwa na katibu wa Bunge.

Kanuni hizo zimesainiwa na Katibu wa Bunge la Tanzania, Nenelwa Mwihambi, Februari 7, 2023.

Mbali na hayo, waandishi wamepangiwa namna ya kuripoti habari za Bunge ambapo kanuni hizo zinayataja mambo ambayo hayataruhusiwa kuripotiwa ni yale ya faragha.

Kanuni hizo zinasema masuala hayo ni yale ambayo habari zake zikitolewa kwa waandishi wa habari kabla ya wakati wake zinaweza kuathiri uamuzi wa kamati na pia kusababisha ukiukwaji wa kanuni za Bunge.

Masuala hayo ni kazi zote zinazopelekwa kwenye Kamati na Spika ili kupata mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa na Bunge na shughuli zote za uchambuzi wa hoja mbalimbali zilizoko mbele ya kamati.

Mengine ni shughuli zote zinazotekelezwa kwa utaratibu wa kiuchunguzi, shughuli zote za kiuchunguzi zenye utaratibu uliowekewa masharti zinazotekelezwa na kamati na shughuli zote zinazotekelezwa na kamati ndogo na kamati zinapofanya ziara za kiuchunguzi.

Kanuni hizo zimetaja kamati zinazotekeleza majukumu kwa faragha ni Kamati ya Uongozi, Kamati ya Kanuni za Bunge, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Kamati ya Hesabu ya Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Bajeti.

Pia, inasema taarifa zenye uwazi wenye mipaka kuwa ni taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inapowasilishwa bungeni inakuwa wazi kwa vyombo vya habari.

Taarifa nyingine ni mchakato wa kamati hizi kuwahoji maofisa masuuli kuhusiana na taarifa ya CAG utakuwa wazi hadi hatua ambayo Kamati inataka kufanya uamuzi wa kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa na Bunge, ambapo Kamati itafanya kazi zake kwa faragha.

Kanuni hizo zimesema iwapo mchakato wa kuhoji maofisa masuhuli unaofanywa utakuwa ni wa kiuchunguzi, mchakato utafanyika kwa faragha.

Kuhusu upigaji wa picha, kanuni hizo zimesema upigaji wa picha katika ukumbi wa Bunge na maeneo ya Bunge utazingatia heshima, utu na staha.

Pia alisema vifaa vitakavyotumika katika upigaji picha vitaidhinishwa na Katibu kabla ya kupiga picha katika ukumbi wa Bunge na maeneo ya Bunge.

“Mpiga picha atakapokuwa kwenye ukumbi wa Bunge ataelekeza kamera yake kwa Spika au Mbunge anayezungumza wakati huo,”zilisema kanuni hizo.

Pia mpiga picha anaweza kuacha kuelekeza kamera kwa Spika au Mbunge na kuelekeza sehemu nyingine pale ambapo kuna tukio jingine linalohusiana na shughuli inayoendelea.

Aidha, kanuni hizo zimetaja maeneo yasiyoruhusiwa kupiga picha ni maeneo ya ukaguzi wa usalama, benki, mgahawa, zahanati ya Bunge, maegesho ya magari, kumbi zote za kupumzikia wageni na jengo la utawala na mengine yatakayoamuliwa na Katibu.

Hata hivyo, upigaji picha katika maeneo hayo unaweza kuruhusiwa kwa kibali kitakachotolewa na Katibu.
Kanuni hizo zimesema chombo cha habari au mtu atakayekiuka mwongozo huu anaweza kuchukuliwa hatua za onyo na kusimamishwa kwa muda kuchukua na kutoa habari za Bunge.

Pia zimeeleza hatua nyingine ni kufutiwa kibali cha ukusanyaji wa habari na utoaji wa habari za Bunge.

Aidha, kanuni hizo zimesema mtu au chombo cha habari kitakachokiuka masharti ya mwongozo huo kitapata fursa ya kusikilizwa na katibu kabla ya kuchukuliwa hatua.

Kutokana na kanuni hizo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wakariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile alisema, “tumesikia, tutazichambua, tutawasiliana na uongozi wa Bunge na kwa nini tunataka kurudisha nyuma uhuru wa habari.”

Naye Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari ya Dodoma (CPC), Mussa Yusuph alisema ameshtushwa na hizo kanuni kutokana na kutungwa wakati serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imejipambanua katika kutanua wigo wa masuala ya kidemokrasia na uhuru wa kujieleza.

Amesema Rais Samia aliweza kufungua vyombo vya habari vilivyofungwa, kupunguza ada za usajili katika mitandao ya kijamii lakini wakati huo huo kuna taasisi nyingine zinakuja na mitizamo ambayo inaaminika ni kurejesha nyuma jitihada za Rais Samia.

“Mimi maoni yangu kanuni hizo zirejewe upya na kama kulikuwa na mtizamo uliosababisha kuja kwa hizo kanuni, wanaweza kufungua meza ya majadiliano na upande wetu (waandishi wa habari) tukaja na kanuni ambazo zitakuwa rafiki,” amesema.

Amesema kanuni rafiki zitawezesha kuwapasha vyema wananchi kuhusu kinachoendelea bungeni kwasababu chombo hicho ni mali yao.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading