Bunge latunga kanuni ngumu kwa wanahabari, wadau wang’aka

Dodoma. Bunge la Tanzania limetunga Kanuni mpya za mwaka 2023, ambazo zimeweka adhabu kwa waandishi wa habari na masharti ya namna ya kupiga picha ndani ya ukumbi wa Bunge.

Kanuni hizo ambazo zimechapishwa katika Gazeti la Serikali (GN) ya Machi 21, 2023 zimeeleza maeneo yanayoruhusiwa kupiga picha na kamera zitakazotumika zitalazimika kuruhusiwa na katibu wa Bunge.

Kanuni hizo zimesainiwa na Katibu wa Bunge la Tanzania, Nenelwa Mwihambi, Februari 7, 2023.

Mbali na hayo, waandishi wamepangiwa namna ya kuripoti habari za Bunge ambapo kanuni hizo zinayataja mambo ambayo hayataruhusiwa kuripotiwa ni yale ya faragha.

Kanuni hizo zinasema masuala hayo ni yale ambayo habari zake zikitolewa kwa waandishi wa habari kabla ya wakati wake zinaweza kuathiri uamuzi wa kamati na pia kusababisha ukiukwaji wa kanuni za Bunge.

Masuala hayo ni kazi zote zinazopelekwa kwenye Kamati na Spika ili kupata mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa na Bunge na shughuli zote za uchambuzi wa hoja mbalimbali zilizoko mbele ya kamati.

Mengine ni shughuli zote zinazotekelezwa kwa utaratibu wa kiuchunguzi, shughuli zote za kiuchunguzi zenye utaratibu uliowekewa masharti zinazotekelezwa na kamati na shughuli zote zinazotekelezwa na kamati ndogo na kamati zinapofanya ziara za kiuchunguzi.

Kanuni hizo zimetaja kamati zinazotekeleza majukumu kwa faragha ni Kamati ya Uongozi, Kamati ya Kanuni za Bunge, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Kamati ya Hesabu ya Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Bajeti.

Pia, inasema taarifa zenye uwazi wenye mipaka kuwa ni taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inapowasilishwa bungeni inakuwa wazi kwa vyombo vya habari.

Taarifa nyingine ni mchakato wa kamati hizi kuwahoji maofisa masuuli kuhusiana na taarifa ya CAG utakuwa wazi hadi hatua ambayo Kamati inataka kufanya uamuzi wa kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa na Bunge, ambapo Kamati itafanya kazi zake kwa faragha.

Kanuni hizo zimesema iwapo mchakato wa kuhoji maofisa masuhuli unaofanywa utakuwa ni wa kiuchunguzi, mchakato utafanyika kwa faragha.

Kuhusu upigaji wa picha, kanuni hizo zimesema upigaji wa picha katika ukumbi wa Bunge na maeneo ya Bunge utazingatia heshima, utu na staha.

Pia alisema vifaa vitakavyotumika katika upigaji picha vitaidhinishwa na Katibu kabla ya kupiga picha katika ukumbi wa Bunge na maeneo ya Bunge.

“Mpiga picha atakapokuwa kwenye ukumbi wa Bunge ataelekeza kamera yake kwa Spika au Mbunge anayezungumza wakati huo,”zilisema kanuni hizo.

Pia mpiga picha anaweza kuacha kuelekeza kamera kwa Spika au Mbunge na kuelekeza sehemu nyingine pale ambapo kuna tukio jingine linalohusiana na shughuli inayoendelea.

Aidha, kanuni hizo zimetaja maeneo yasiyoruhusiwa kupiga picha ni maeneo ya ukaguzi wa usalama, benki, mgahawa, zahanati ya Bunge, maegesho ya magari, kumbi zote za kupumzikia wageni na jengo la utawala na mengine yatakayoamuliwa na Katibu.

Hata hivyo, upigaji picha katika maeneo hayo unaweza kuruhusiwa kwa kibali kitakachotolewa na Katibu.
Kanuni hizo zimesema chombo cha habari au mtu atakayekiuka mwongozo huu anaweza kuchukuliwa hatua za onyo na kusimamishwa kwa muda kuchukua na kutoa habari za Bunge.

Pia zimeeleza hatua nyingine ni kufutiwa kibali cha ukusanyaji wa habari na utoaji wa habari za Bunge.

Aidha, kanuni hizo zimesema mtu au chombo cha habari kitakachokiuka masharti ya mwongozo huo kitapata fursa ya kusikilizwa na katibu kabla ya kuchukuliwa hatua.

Kutokana na kanuni hizo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wakariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile alisema, “tumesikia, tutazichambua, tutawasiliana na uongozi wa Bunge na kwa nini tunataka kurudisha nyuma uhuru wa habari.”

Naye Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari ya Dodoma (CPC), Mussa Yusuph alisema ameshtushwa na hizo kanuni kutokana na kutungwa wakati serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imejipambanua katika kutanua wigo wa masuala ya kidemokrasia na uhuru wa kujieleza.

Amesema Rais Samia aliweza kufungua vyombo vya habari vilivyofungwa, kupunguza ada za usajili katika mitandao ya kijamii lakini wakati huo huo kuna taasisi nyingine zinakuja na mitizamo ambayo inaaminika ni kurejesha nyuma jitihada za Rais Samia.

“Mimi maoni yangu kanuni hizo zirejewe upya na kama kulikuwa na mtizamo uliosababisha kuja kwa hizo kanuni, wanaweza kufungua meza ya majadiliano na upande wetu (waandishi wa habari) tukaja na kanuni ambazo zitakuwa rafiki,” amesema.

Amesema kanuni rafiki zitawezesha kuwapasha vyema wananchi kuhusu kinachoendelea bungeni kwasababu chombo hicho ni mali yao.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit

Dar es Salaam — Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has declared an outbreak of Marburg virus, confirming a single case in the northwestern region of Kagera after a meeting with WHO director-general Tedros Adhanom Ghebreyesus.

The confirmation follows days of speculation about a possible outbreak in the region, after the WHO reported a number of deaths suspected to be linked to the highly infectious disease.

While Tanzania’s Ministry of Health declared last week that all suspected cases had tested negative for Marburg, the WHO called for additional testing at international reference laboratories.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”Amelia Clemence, public health researcher

Subsequent laboratory tests conducted at Kagera’s Kabaile Mobile Laboratory and confirmed in Dar es Salaam identified one positive case, while 25 other suspected cases tested negative, the president told a press conference in Dodoma, in the east of the country today (Monday).

“The epicentre has now shifted to Biharamulo district of Kagera,” she told the press conference, distinguishing this outbreak from the previous one centred in Bukoba district.

Tedros said the WHO would release US$3 million from its emergencies contingency fund to support efforts to contain the outbreak.

Health authorities stepped up surveillance and deployed emergency response teams after the WHO raised the alarm about nine suspected cases in the region, including eight deaths.

The suspected cases displayed symptoms consistent with Marburg infection, including headache, high fever, diarrhoea, and haemorrhagic complications, according to the WHO’s alert to member countries on 14 January. The organisation noted a case fatality rate of 89 per cent among the suspected cases.

“We appreciate the swift attention accorded by the WHO,” Hassan said.

She said her administration immediately investigated the WHO’s alert.

“The government took several measures, including the investigation of suspected individuals and the deployment of emergency response teams,” she added.

Cross-border transmission

The emergence of this case in a region that experienced Tanzania’s first-ever Marburg outbreak in March 2023 has raised concerns about cross-border transmission, particularly following Rwanda’s recent outbreak that infected 66 people and killed 15 before being declared over in December 2024.

The situation is particularly critical given Kagera’s position as a transport hub connecting four East African nations.

Amelia Clemence, a public health researcher working in the region, says constant vigilance is required.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”

The Kagera region’s ecosystem, home to fruit bats that serve as natural reservoirs for the Marburg virus, adds another layer of complexity to disease surveillance efforts.

The virus, closely related to Ebola, spreads through contact with bodily fluids and can cause severe haemorrhagic fever.

Transparency urged

Elizabeth Sanga, shadow minister of health for Tanzania’s ACT Wazalendo opposition party, says greater transparency would help guide public health measures.

“This could have helped to guide those who are traveling to the affected region to be more vigilant and prevent the risk of further spread,” she said.

WHO regional director for Africa Matshidiso Moeti says early notification of investigation outcomes is important.

“We stand ready to support the government in its efforts to investigate and ensure that measures are in place for an effective and rapid response,” she said, noting that existing national capacities built from previous health emergencies could be quickly mobilised.

The situation coincides with leadership changes in Tanzania’s Ministry of Health, with both the chief medical officer and permanent secretary being replaced.

This piece was produced by SciDev.Net’s Sub-Saharan Africa English desk.

Source: allafrica.com

Continue Reading