Bomba la Tazama kupanuliwa, Tanzania, Zambia wajadiliana

Bomba la Tazama kupanuliwa, Tanzania, Zambia wajadiliana

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Nishati na ile ya Zambia zipo katika mazungumzo yanayolenga kuongeza uwekezaji katika bomba la Mafuta la Tanzania – Zambia (TAZAMA).

Mazungumzo hayo yanalenga kupanua bomba la mafuta kutoka inchi 8 hadi inchi 12 ili kuliwezesha kuwa na uwezo wa kusafirisha mafuta mengi zaidi kwenda nchini Zambia na nchi nyingine za jirani.

Mbali na hilo, pia zipo katika mkakati wa kujenga bomba jipya litakalokuwa na inchi 24 ili kuongeza usafirishaji.

Hayo yameelezwa leo Jumatatu, Agosti 26, 2024 wakati Serikali ikipokea gawio la Sh4.35 bilioni kutoka Tazama Pipeline ikiwa ni sehemu ya faida waliyotengeneza.

Akizungumza baada ya kupokea gawio hilo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko amesema lengo la kufanya uwekezaji huo sasa ni kushusha gharama kwa wamiliki wa vituo vya mafuta katika maeneo ambayo bomba linapita.

“Mbali na upanuzi pia tunatarajia kuanza ujenzi wa bomba jipya la inchI 24 na hili lipo katika hatua za ununuzi kabla utekelezaji haujaanza,” amesema Dk Biteko.

Amesema lengo ni kuona utumiaji wa malori katika kusafirisha mafuta unapungua na watu wengi wanahamia katika kutumia bomba kwa kuchukua mafuta katika baadhi ya vituo vitakavyowekwa katika mikoa husika.

“Lengo letu ni mafuta yanayokwenda mikoa ya kusini kwa kutumia malori,  yasafirishwe kwa bomba,” amesema Dk Biteko.

Amesema kufanya hivyo kunalenga kuhakikisha Watanzania wanapata mafuta kwa bei nafuu kwa sababu gharama za usafirishaji, ni miongoni mwa vitu vinavyochangia kuongezeka kwa bei ya mafuta ya rejareja.

Pia, kufanya hivyo kutasaidia kulinda barabara zisiharibike haraka kutokana na usafirishaji unaofanywa kwa kutumia malori.

Akizungumzia gawio hilo, Dk Biteko amesema ni moja ya hatua njema ambayo inatia moyo. Amesema Rais Samia Suluhu Hassan alipofanya ziara nchini Zambia moja ya maelekezo aliyotoa ni kuhakikisha miradi inayotekelezwa na nchi hizo mbili ina inasimamiwa ili kuleta manufaa.

“Pia miradi hii ichangie katika kubadilisha maisha ya watu na hali zao na kwa sababu tulikuwa hatujapata gawio tangu mwaka 2019, niliwaita nikawauliza wakasema wataleta hela na leo wameleta,” amesema Dk Biteko.

Akifafanua kuhusu ujenzi wa bomba jipya, Mkurugenzi Mtendaji wa Tazama, Davison Thawethe amesema bomba hilo jipya litakuwa na uwezo wa kusafirisha futi za ujazi milioni tano za mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Ndola Zambia kwa mwaka.

“Tumeagiza kampuni kufanya upembuzi yakinifu utakaoanza siku yoyote kuanzia sasa ili kubaini bomba hilo litagharimu kiasi gani,” amesema.

Amesema uamuzi wa kujenga bomba jipya ni kuendana na ukuaji wa bidhaa za mafuta unaoongezeka kila mwaka.

Awali, Mwenyekiti wa bodi wa kampuni hiyo, Peter Mumba amesema gawio hilo limetokana na utendaji mzuri walioushuhudia licha ya baadhi ya changamoto walizopitia.

“Jambo hilo limefanya kuboresha utoaji wetu wa huduma, jitihada hizi hazijaimarisha uhudumiaji wateja tu bali pia uwezo wetu wa kifedha,” amesema Mumba.

Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu amesema shirika la Tazama lilianza miaka 58 iliyopita na kama ingekuwa ni umri wa mtu basi amebakiza miaka miwili kabla hajastaafu.

Amesema kipindi hicho mtu huwa ameishiwa nguvu ila ni tofauti na Tazama ambao umri huo ndiyo wanaanza kuamka na kupata nguvu kubwa.

Amesema fedha hizo zitakwenda kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kama ilivyoelekezwa.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading