Bomba la Tazama kupanuliwa, Tanzania, Zambia wajadiliana

Bomba la Tazama kupanuliwa, Tanzania, Zambia wajadiliana

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Nishati na ile ya Zambia zipo katika mazungumzo yanayolenga kuongeza uwekezaji katika bomba la Mafuta la Tanzania – Zambia (TAZAMA).

Mazungumzo hayo yanalenga kupanua bomba la mafuta kutoka inchi 8 hadi inchi 12 ili kuliwezesha kuwa na uwezo wa kusafirisha mafuta mengi zaidi kwenda nchini Zambia na nchi nyingine za jirani.

Mbali na hilo, pia zipo katika mkakati wa kujenga bomba jipya litakalokuwa na inchi 24 ili kuongeza usafirishaji.

Hayo yameelezwa leo Jumatatu, Agosti 26, 2024 wakati Serikali ikipokea gawio la Sh4.35 bilioni kutoka Tazama Pipeline ikiwa ni sehemu ya faida waliyotengeneza.

Akizungumza baada ya kupokea gawio hilo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko amesema lengo la kufanya uwekezaji huo sasa ni kushusha gharama kwa wamiliki wa vituo vya mafuta katika maeneo ambayo bomba linapita.

“Mbali na upanuzi pia tunatarajia kuanza ujenzi wa bomba jipya la inchI 24 na hili lipo katika hatua za ununuzi kabla utekelezaji haujaanza,” amesema Dk Biteko.

Amesema lengo ni kuona utumiaji wa malori katika kusafirisha mafuta unapungua na watu wengi wanahamia katika kutumia bomba kwa kuchukua mafuta katika baadhi ya vituo vitakavyowekwa katika mikoa husika.

“Lengo letu ni mafuta yanayokwenda mikoa ya kusini kwa kutumia malori,  yasafirishwe kwa bomba,” amesema Dk Biteko.

Amesema kufanya hivyo kunalenga kuhakikisha Watanzania wanapata mafuta kwa bei nafuu kwa sababu gharama za usafirishaji, ni miongoni mwa vitu vinavyochangia kuongezeka kwa bei ya mafuta ya rejareja.

Pia, kufanya hivyo kutasaidia kulinda barabara zisiharibike haraka kutokana na usafirishaji unaofanywa kwa kutumia malori.

Akizungumzia gawio hilo, Dk Biteko amesema ni moja ya hatua njema ambayo inatia moyo. Amesema Rais Samia Suluhu Hassan alipofanya ziara nchini Zambia moja ya maelekezo aliyotoa ni kuhakikisha miradi inayotekelezwa na nchi hizo mbili ina inasimamiwa ili kuleta manufaa.

“Pia miradi hii ichangie katika kubadilisha maisha ya watu na hali zao na kwa sababu tulikuwa hatujapata gawio tangu mwaka 2019, niliwaita nikawauliza wakasema wataleta hela na leo wameleta,” amesema Dk Biteko.

Akifafanua kuhusu ujenzi wa bomba jipya, Mkurugenzi Mtendaji wa Tazama, Davison Thawethe amesema bomba hilo jipya litakuwa na uwezo wa kusafirisha futi za ujazi milioni tano za mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Ndola Zambia kwa mwaka.

“Tumeagiza kampuni kufanya upembuzi yakinifu utakaoanza siku yoyote kuanzia sasa ili kubaini bomba hilo litagharimu kiasi gani,” amesema.

Amesema uamuzi wa kujenga bomba jipya ni kuendana na ukuaji wa bidhaa za mafuta unaoongezeka kila mwaka.

Awali, Mwenyekiti wa bodi wa kampuni hiyo, Peter Mumba amesema gawio hilo limetokana na utendaji mzuri walioushuhudia licha ya baadhi ya changamoto walizopitia.

“Jambo hilo limefanya kuboresha utoaji wetu wa huduma, jitihada hizi hazijaimarisha uhudumiaji wateja tu bali pia uwezo wetu wa kifedha,” amesema Mumba.

Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu amesema shirika la Tazama lilianza miaka 58 iliyopita na kama ingekuwa ni umri wa mtu basi amebakiza miaka miwili kabla hajastaafu.

Amesema kipindi hicho mtu huwa ameishiwa nguvu ila ni tofauti na Tazama ambao umri huo ndiyo wanaanza kuamka na kupata nguvu kubwa.

Amesema fedha hizo zitakwenda kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kama ilivyoelekezwa.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Popular
Swahili News Editor

MGAO WA MAJI WAWATESA WAZANZIBARI

Wananchi wengi hasa katika maeneo ya Mjini Unguja, wanalalamikia ukosefu wa maji safi na salama huku Mamlaka ya Maji Zanzibar ikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ujuzi na wataalam katika masuala ya uandisi wa Maji na fani nyengine.Continue Reading