Ngariba wanapovuka mipaka kukeketa mabinti -3
Mpaka wa Sirari wilayani Tarime, mkoani Mara umekuwa ukitumiwa na ngariba kuvuka kati ya Tanzania na Kenya kutekeleza vitendo vya ukeketaji.Continue Reading
Mpaka wa Sirari wilayani Tarime, mkoani Mara umekuwa ukitumiwa na ngariba kuvuka kati ya Tanzania na Kenya kutekeleza vitendo vya ukeketaji.Continue Reading
Aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni (CCM) na Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, Dk Faustine Ndugulile anatarajiwa kuzikwa Jumanne ya Desemba 3, 2024 katika makaburi ya Mwongozo yaliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.Continue Reading
Unguja. Licha ya kuwa na kituo cha afya kilichojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf), wajawazito wa visiwa vya Uzi na Ng’ambwa Mkoa wa Kusini Unguja, wanaendelea kusotea huduma za uzazi kutokana na ukosefu wa madaktari na wauguzi kwa takribani mwaka mmoja sasa.
Ng’ambwa ina wakazi 1,158 kati ya hao wanawake ni 571 na wanaume 587, huku Uzi ikiwa na wakazi 3,075 kati ya hao wanawake ni 1,510 na wanaume 1,565. Wote wanategemea kituo hicho cha afya kilichopo Kisiwa cha Uzi kwa ajili ya huduma.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Ahmed Suleiman Abdulla aliahidi siku ya ufunguzi wa kituo hicho wakati wa shamrashamra za Mapinduzi Desemba 27, 2023 kuwa kitapelekewa wataalamu wa afya.
Daktari dhamana (mganga mfawidhi) wa kituo hicho cha afya, Saleh Lilah Ali akizungumza na Mwananchi Novemba 25, 2024 ameeleza ugumu wanaokumbana nao katika utoaji huduma, akikiri kuwapo uchache wa wafanyakazi kwamba kuna muuguzi mmoja na daktari mmoja ambaye ni yeye.
Daktari huyo pamoja na muuguzi hawaishi kwenye visiwa hivyo, bali huenda kutoa huduma na kuondoka.
“Changamoto ni nyingi tunajua wanawake wapo na wanajifungua nyumbani, hawezi kuja hapa kwa sababu ya uchache wa wafanyakazi na hatuwezi kutoa huduma saa 24 kwa sababu ya uchache huohuo,” amesema Dk Saleh akiiomba Serikali iongeze wafanyakazi.
Amesema kwa mwezi mmoja wanafikisha wastani watu 300 hadi 500 wanaopatiwa huduma katika kituo hicho.
Kwa upande wa watoto, amesema wanafika takribani 100, huku wajawazito wanaohudumiwa wakikadiriwa kufikia 60 kwa mwezi.
Ili kutoa huduma nzuri kulingana na wananchi wanaohitaji huduma katika kituo hicho, Dk Saleh amesema angalau kwa uchache wanahitajika wauguzi watano na madaktari watatu.
Kwa mujibu wa miongozo ya Shirika la Afya Dunia (WHO), muuguzi mmoja anatakiwa ahudumie wajawazito wasiozidi watano.
Dk Saleh amesema wanawaelekeza wajawazito wanaofika wakati wa kujifungua, waondoke kisiwani humo kutafuta sehemu ya kuishi karibu na hospitali ambako watapata huduma zote kwa usalama.
Walichosema wanawake
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wanawake wakazi wa visiwa hivyo wamesema wanapata huduma za kujifungua Kitogani au Unguja Ukuu lakini wanakumbana na kikwazo cha barabara kwani kuna daraja ambalo halipitiki muda wote kutokana na maji kujaa na kuondoka kulingana na mfumo wa bahari.
Asha Said Ali, mkazi wa Uzi amesema: “Tunapata matatizo kila kukicha, mwanangu hivi majuzi alikuwa mjamzito, alipata uchungu nikaja naye hapa nikaambiwa niondoke naye twende Unguja Ukuu, nilipofika huko nikaambiwa nimpeleke Kitogani.
“Hapo nilisikia akili yangu kuchanganyikiwa, na uchungu tunaujua sote kina mama jinsi unavyouma, inakuwa tafrani tupu,” amesema.
Ashura Said, amesema: “Kutokana na hali hii, nimeshawazalisha wanawake watano wakiwa nyumbani kwa nyakati tofauti, hiyo ni hatari lakini ndiyo hivyo tunamuomba Mungu. Utafanyaje, inabidi ufanye hivyo kwa kubahatisha tukizidi kumuomba Mungu alete usalama.”
“Nimewahi kumzalisha mama mmoja kwenye gari wakati tunampeleka Unguja Ukuu, tulipofika kwenye daraja tukakuta maji yameshajaa, hatukuwahi kuvuka, kwa hiyo akajifungua kwenye gari lakini tunashukuru Mungu alijifungua salama,” amesema.
Hajiram Ramadhan Aidar, amesema kujifungulia nyumbani unapoteza damu nyingi na kuongeza: “Sasa hapo kuna mawili, kupoteza maisha au kunusurika.”
Mwinzuma Arah Khamis kutoka Shehia ya Ng’ambwa, naye amesema ameshawahi kuwasaidia wajawazito kujifungua.
“Kwa sisi wanawake wa huku ni changamoto kubwa, ukifika wakati wa kujifungua unaambiwa nenda mjini ili siku ya kujifungua uwe salama, lakini kama una watoto wengine roho yako inakuwa ngumu kukaa huko huku nyumbani hujui watoto wako wanaishije. Ndiyo maana unabahatisha unasubiri uchungu uje ndipo uondoke au wakati mwingine watu wanaamua kuzalia nyumbani,” amesema.
Wanaeleza kutokana na vipato vyao, wanapata changamoto kugharimia nauli za kufuata huduma ng’ambo.
“Ukichukua bodaboda, watu wawili mnalipa Sh8, 000 kama ni boti mnalipa Sh10, 000, lakini mjamzito kumpandisha kwenye pikipiki na njia yenyewe ilivyo mbovu unamwongezea uchungu mara mbili,” amesema Mwinzuma.
Mashavu Mabrouk Khamis, amesema kwa kuwa kuna tatizo la uhaba wa madaktari na wauguzi, Serikali iwaruhusu wakunga wazalishe lakini iwapatie mafunzo angalau ya miezi mitatu ili wapate ujuzi.
Amesema wakati wa kufungua kituo hicho waliahidiwa kupewa wataalamu wote lakini wanasikitika kuona ahadi haijatekelezwa.
Maliki Mbaraka Makame, amesema wataalamu wawili waliopo hawaishi katika kisiwa hicho bali hufika na kuondoka ilhali kuna nyumba kwa ajili yao.
“Sijaona mpaka sasa madaktari wakikaa hapa, wanakuja na kuondoka hatujui kwa nini inakuwa hivyo. Serikali inatakiwa iwaajiri wazawa wa hapa kijijini, hili litapunguza adha hii ya wataalamu kutokaa hapa,” amesema.
Ahmed Ali Mussa, mkazi wa Shehia ya Ng’ambwa amesema baadhi ya wanawake hawana ndugu nje ya kisiwa hicho, hivyo hushindwa kuondoka wakati wa kujifungua.
Shekha wa Shehia ya Uzi, Othman Mwinyi Haji amesema changamoto hiyo imekuwa ya muda mrefu licha ya kujengewa kituo hicho kipya bado kilio ni kilekile.
Amesema tangu kituo hicho kifunguliwe mpaka sasa ni mwaka mmoja lakini huduma zinazorota wakati mwingine wataalamu hao wanashindwa kufika kwa sababu ya maji kujaa kwenye daraja.
“Akikuta maji yamejaa anasubiri mpaka yatoke, kama yamejaa saa mbili asubuhi basi mpaka yatoke inakuwa saa nane mchana, kwa hiyo hawezi tena kuja, huku kwanza hata muda wenyewe wa kufunga kituo unakuwa umeshafika,” amesema.
Othman amesema: “Hivi karibuni mjamzito alijifungua akiwa kwenye fiber (boti) anapelekwa Unguja Ukuu, hata yule nahodha alipoona mwanamke huyo kazidiwa akaanza kujifungua, alichumpa (kuruka) ili kuwaachia wanawake wamshughulikie.”
Ameiomba Serikali iwapatie wauguzi na madaktari ambao watahudumia wananchi kwa saa 24, akieleza kituo hicho pamoja na changamoto zilizopo kinafungwa saa 9.00 alasiri.
Amesema suala la wajawazito kulazimika kwenda kwa ndugu wanapofika hatua ya kujifungua inawapa kero.
“Kuna ndugu hawapendi kukaa na watu ila mtu anamkubalia kwa sababu ya muhali tu ila kiuhalisia inakosesha amani,” amesema.
Amesema iwapo kungekuwa na njia nzuri ingewasaidia hata inapotokea dharura kuwahi kwenda ngambo katika vituo vya afya vingine.
DMO aeleza
Akizungumzia hali hiyo, Daktari Dhamana (Mganga Mkuu) wa Wilaya ya Kati Unguja, Dk Amina Hussein Pandu amesema Serikali inajipanga kuwezesha ktuo hicho kutoa huduma.
“Kitu kimoja kikubwa cha kufanya ni kuwa na gari na boti ya dharura na itafutiwe sehemu ya kukaa, hivyo ndiyo vitu wizara inajipanga navyo,” amesema.
Amesema vituo vina madaraja na hicho bado kipo katika daraja la kwanza ila kikifika la pili kitaweza kutoa huduma zote.
“Serikali inajipanga, tunaomba wawe wastahimilivu waipe muda, bado inaweka mazingira kwa kina mama. Kwa sasa kinachotakiwa angalau kuwa na boti na gari la dharura ili mama akipata uzazi pingamizi aweze kusafirishwa,” amesema.
Dk Amina amesema kituo hicho hakina uhaba wa watumishi kwa kuwa wameshapelekwa. Hata hivyo, hakuwa na jibu la moja kwa moja la idadi ya waliopelekwa na jumla ya wataalamu waliopo katika kituo hicho kwa sasa.
Kuhusu wataalamu hao kukaa kisiwani humo, amesema hawana amri ya kumlazimisha kukaa kwenye nyumba hizo kwa sababu wengine wanafamilia zao nje ya Uzi.
Kuhusu wakunga kuruhusiwa kuzalisha, Dk Amina amesema: “Wakunga wa wajadi kwa sasa tunawaomba wawapeleke wajawazito kituo cha afya ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea.”
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk Khalid Mohamed Salum amesema tayari Serikali ipo kwenye mchakato wa kuweka miundombinu ya barabara na ujenzi wa daraja katika eneo hilo.
Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 8.72 na daraja likiwa na urefu wa kilomita mbili na upana wa mita 6.5 litaweza kupitisha magari mawili kwa pamoja.
Pia kutakuwa na njia ya waenda kwa miguu na reli za kuzuia ajali. Daraja hilo amesema litakuwa na urefu wa mita nne na nusu kwenda juu.
Amesema Sh35 bilioni zitatumika katika ujenzi wa barabara na daraja hilo, hivyo kuondoa changamoto hiyo ya muda mrefu.Continue Reading
Dodoma. Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imewataka watu wanaomba mikopo kidijitali, kusoma maelekezo vizuri ili kuepuka kuruhusu kampuni hizo kuingia katika orodha ya namba za simu (phone book) na kuwadhalilisha.
Kauli hiyo imekuja wakati baadhi ya kampuni zinazotoa mikopo kwa njia ya kidijitali, kutuma ujumbe mfupi wa maneno unaodhalilisha na wakati mwingine kutuma picha za vitambulisho vya wanaowadai.
Hatua hiyo imekuwa ikiibua malalamiko kwa jamii na hadi imekuibuliwa bungeni ambapo Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson alionyesha kukerwa na udhalilishaji unaofanywa kwa kuwashirikisha wasiohusika na mikopo hiyo.
Spika Tulia alieleza hayo Juni 27, 2024, bungeni wakati wa kipindi cha maswali na majibu akiitaka Serikali ieleze suala hilo ambalo lilikuwa likijadiliwa zaidi nje ya Bunge, “sijui kama kuna mwongozo wowote na Serikali mnalipokea na mnalifanyia kazi, hilo limekuaje.”
Aliyekuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye alijibu suala hilo akikiri kuwepo kwa changamoto hiyo ya watu ambao wanakopeshana mitandaoni na baadaye wanatuma taarifa kwa watu wanaomzunguka mkopaji.
Nape alisema Serikali imeiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na Kitengo cha Kudhibiti Wizi Mtandaoni na Jeshi la Polisi kulifanyia kazi.
Aprili 1, 2024 Mwananchi iliripoti malalamiko ya baadhi ya watu wanaotumiwa ujumbe wa kuwataka kuwakumbusha waliokopa kulipa madeni yao, na jinsi kampuni zinavyopata namba hizo za simu.
“Ndugu wa karibu/jamaa/rafiki/jirani wa (jina la mkopaji na namba ya simu) aliyechukua mkopo kwa nia ya mtandao kupitia application ya… unafahamishwa kuwa mtu huyu amekiuka makubaliano kwa kutolipa deni siku husika ya marejesho na kutopokea simu za ofisi, hivyo tutamchukulia hatua kwa kosa hilo.
“Unaombwa kumpigia simu muhusika na kumjulisha kuwa ana masaa mawili ya kulipa deni kabla ya hatua kali hazijachukuliwa dhidi yake. Fanya hivyo kuepuka usumbufu.”
Leo Jumatatu, Novemba 25, 2024, Mkurugenzi Mkuu wa PDPC, Dk Emmanuel Mkilia akizungumzia maandalizi ya warsha ya kuongeza uelewa kuhusu dhana ya ulinzi wa taarifa binafsi jijini Dodoma amegusia suala hilo la udhalilishaji.
“Kimsingi tumeona kuna uvunjifu mkubwa wa sheria ya ulinzi wa Taifa, hasa watu wanaotumia mitandao wanapata nafasi kutumia picha na vitambulisho vya watu na wanatumia sms (ujumbe mfupi wa maneno) kwa watu wote walioko ndani ya simu husika hilo ni kosa kisheria,” amesema.
Amesema suala hilo wamekuwa wakilishughulikia kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kuhakikisha taasisi ndogo za fedha ziwe zimesajiliwa kisheria na BoT.
Amesema wanaofanya biashara hiyo wanatakiwa kuzingatia sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi na ndio maana wengi wamefungiwa hivi karibuni kujishughulisha na biashara hiyo.
Amesema mwananchi anapoomba mkopo kupitia programu tumizi ‘application’ hizo kwa kujua ama kwa kutokujua inakuwa ni sharti kama hutalipa deni hilo ambalo wanawataka aruhusu ili waweze kuingia kwenye orodha ya namba za simu (phone book) na kuangalia anwani ya watu unaowasiliana nao.
Dk Mkilia amesema bila kujua mwananchi anapoweka alama ya tiki, application hiyo inakuwa na ruhusa ya kuingia katika orodha ya namba za simu, hivyo hata wakati mwingine kabla ya muda wa kulipa kufika taarifa zinapelekwa za kumkashifu huyo mtu kwa watu wote anawasiliana nao.
“Kuwaasa wananchi kupitia vizuri maelekezo yanayoelekezwa mle ile usijikute kuwa ni mwathirika,” amesema.
Tayari BoT imezifungia kutoa mikopo programu tumizi (application) 69 baada ya kuzibaini zinaendesha shughuli hiyo kidijitali bila kuwa na leseni wala idhini.
BoT ilitangaza uamuzi huo Novemba 21, 2024 kupitia taarifa iliyosainiwa na Gavana wa Bot, Emmanuel Tutuba ikiutahadharisha umma wa Watanzania kutojihusisha na majukwaa na programu tumizi zilizofungiwa.
Kuhusu warsha ya kuongeza uelewa juu ya dhana ya ulinzi wa taarifa binafsi, Dk Mkilia amesema warsha hiyo itafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Desemba 17 hadi 18, 2024 ambapo washiriki ni maofisa ulinzi wa taarifa binafsi (DPOs) wa taasisi za umma na binafsi.
Amesema lengo ni kuelimisha wadau wa ulinzi wa taarifa binafsi nchini na kutoa elimu pamoja na maarifa muhimu kwa taasisi za umma na binafsi kuhusu utekelezaji wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya mwaka 2022 na kanuni zake.
Dk Mkilia amesema katika kutekeleza agizo la Rais Samia Suluhu Hassan alilolitoa Aprili 3,2024 wakati akizindua tume hiyo taasisi 700 za umma na binafsi zimejisajili katika tume hiyo.
Mwakilishi wa Kampuni ya Hilton Law Group ambao wanashirikiana na PDPC katika warsha hiyo, Wakili Dorothy Ndazi amesema ni muhimu kwa taasisi zote kuelewa wajibu wao kuhusu dhana ya ulinzi wa taarifa binafsi.Continue Reading
Unguja. Ukizinduliwa mpango wa maboresho ya huduma za bandari, Rais wa Zanzibar , Dk Hussein Mwinyi amesema utaleta mageuzi ya kiutendaji na kuondoa urasimu kwa kupeana majukumu kwa kila anayehusika kupitia viashiria vilivyowekwa.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo uliondaliwa na Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kwa kushirikiana na Taasisi ya Tony Blair (TBI) leo Novemba 22, 2024 Ikulu Zanzibar, Rais Mwinyi amezitaka taasisi hizo kuwa tayari kuutekeleza ili ulete tija.
Mpango huo pia unazihusisha wizara tatu za Ujenzi, Biashara na Fedha na taasisi 16.
Dk Mwinyi amesema: “Iwapo kuna mmoja katika mnyororo huo hatimizi wajibu wake, atafanya kazi nzima isiende inavyotakiwa, na itabidi wafanye tathimini kila wakati kupitia viashiria vilivyowekwa na wale ambao watashindwa kutekeleza hilo nitapenda kupata taarifa ili tuchukue hatua stahiki.”
“Endapo taasisi zote zitafanya kama inavyotakiwa hakika tutapata mafanikio makubwa katika nchi yetu, hivi sasa nchi kama za Singapore, Gambia na Kenya wanatumia mfumo huo wa ushirikishwaji na wameweza kupata mafanikio makubwa,” amesema Dk Mwinyi.
Ametaja malengo mengine ya mpango huo ni kurahisiha ushushaji wa makasha, kupunguza muda wa meli kukaa ukutani na kupunguza muda wa meli kukaa nangani, hivyo kupunguza muda wa kutoa mizigo bandarini na kuongeza ukuaji wa uchumi.
Dk Mwinyi amesema Serikali imedhamiria kuendesha huduma za bandari kwa ufanisi zaidi kwa kuzingatia bandari ni mlango mkuu wa uchumi wa nchi.
Amesema mikakati ya Serikali ya ukuzaji uchumi Zanzibar inaendelea kuwawekea wafanyabiashara mazingira mazuri na sasa inatarajia kuanza ujenzi wa bandari jumuishi ya Mangapwani.
“Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote kuendeleza sekta ya bandari nchini na miongoni mwa mipango ni kuimarisha bandari za Malindi, Shumba, Mkoani, Pemba,” amesema.
Amewataa wadau wote zikiwemo kampuni za uendeshaji wa bandari, mamlaka za forodha, mamlaka za udhibiti wa bidhaa zinazoingia bandarini, kampuni za utoaji wa mizigo na mamlaka zinazohusika na ulinzi na usalama bandarini kuwa tayari kutekeleza mpango huu kwa vitendo kufikia malengo yake.
“Unapokuwa na ufanisi wa bandari ambayo ndiyo mlango mkuu wa uchumi bila shaka athari zake zinakuwa kubwa zaidi, kwa hiyo tusiishie kutia saini tuhakikishe tunayatekeleza haya,” amesema.
Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Dk Khalid Mohamed Salim amesema Bandari ya Malindi ni ndogo, ilijengwa mwaka 1920 na wakati huo idadi ya wananchi walikuwa wacheche na mahitaji yalikuwa madogo lakini kwa sasa kila kitu kinaongezeka.
Dk Khalid amesema kipindi cha nyuma kumekuwapo msongamano mkubwa, vifaa vicheche, taaluma ndogo na malalamiko mengi, meli zilikuwa zikichelewa zikikaa nangani kwa zaidi ya siku 32 katika Bandari ya Malindi.
“Kutokana na hali hiyo, wapo baadhi ya watu waliamua kutoleta meli zao Zanzibar na kuzipeleka Mombasa, Kenya nyingine kwenda Dar es Salaam, huku bei ya kuleta makontena Zanzibar ilikuwa kubwa hivyo hali ya maisha ilipanda sana,” amesema.
Amesema baada ya Serikali kuanza kuchukua hatua za kufanya maboresho ya bandari hiyo na kumpa mwendeshaji kampuni ya kigeni kutoka Ufaransa ya AGL, kupitia kampuni tanzu ya Zanzibar Multpurpose Terminal (ZMT) takribani Dola 80 milioni za Marekani (Sh212 bilioni) zimeokolewa.
Amesema fedha hizo zilikuwa zinatumika nje ya Zanzibar kuhudumia usafiri wa makontena na kukaa meli muda mrefu katika Bandari ya Malindi.
“Lakini katika kuongeza ufanisi wa bandari, Rais aliagiza kushirikiana na Taasisi ya Tony Blair kuandaa mpango wa maboresho wa huduma za bandari ambao umeshirikisha wadau wote, zikiwemo kampuni za meli za kigeni za wazawa na watu wa forodha,” amesema.
Amesema mpango huo umeshirikisha watu wote na wameweka viashiria vya utekelezaji mzuri ambao utakuwa na maeneo ya maboresho katika huduma za bandari kwa upande wa baharini na huduma za bandari baada ya meli kufika nangani na kupata ukuta isikae zaidi ya siku tatu, huku ushushaji na upandishaji wa makontena kwa meli kubwa mzunguko wake uwe chini.
Katika kuleta ufanisi zaidi, Dk Khalid amesema wataunda kamati itakayowashirikisha wadau wote watakuwa wakikutana kila baada ya miezi mitatu, miezi sita na mwaka mmoja ambao unakuwa wa kuangalia ufanisi wa jumla.
Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Zanzibar (ZPC), Akif Ali Khamis amesema wataboresha maeneo makubwa manne ambayo ni kuona namna gani ukuta unatumika katika utoaji wa huduma na namna ya kuboresha ufanisi katika kutoa huduma ndani ya saa moja, hivyo kupunguza gharama kwa kadri meli inavyokaa nangani.
Katibu Mkuu wa Mawakala wa Forodha Zanzibar, Ahmed Nassor amesema mpango huo utaondoa changamoto zilizokuwa zinaikumba bandari hiyo.
“Mategemeo yetu ikiwa watashirikishwa wadau wote italeta mafaniko makubwa katika bandari hasa katika eneo la ufungaji na ushushaji wa mizigo, sisi tumeona kutoka makontena saba kwa saa hadi kufika makontena 17 kwa sasa, si kazi ndogo,” amesema.Continue Reading
Serikali kupitia Kampuni ya Meli Tanzania (Tashico), imeanza mchakato wa kujenga meli ya mizigo katika Bahari ya Hindi ikiwa ni mkakati wa kuboresha huduma za usafiri na usafirishaji kwenda mashariki ya mbali.Continue Reading
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imezifungia kutoa mikopo programu tumizi (application) baada ya kuzibaini zinaendesha shughuli hiyo kidijitali bila kuwa na leseni wala idhiniContinue Reading
President Samia Suluhu Hassan has announced that 20 people lost their lives in the Kariakoo building collapse as of Wednesday morning.
The Head of State, who was in Brasilia, Brazil, for the G20 Summit, landed in Dar es Salaam today and went directly to the site of the Kariakoo building collapse.
Speaking at the scene, President Samia expressed sorrow over the lives lost despite the rescue efforts.
“Despite the efforts made by the government and rescuers here and elsewhere, we have still lost some of our fellow citizens.
According to the information I received today, as of 9 a.m., we have lost 20 of our people. The government, in collaboration with the families, has ensured they are laid to rest with dignity,” she said.
On Tuesday, President Samia Suluhu Hassan announced an additional 24 hours to rescue people trapped in a collapsed building at Kariakoo in Dar es Salaam.
President Samia expressed optimism that, with divine intervention, some victims might still be found alive beyond this period, despite the standard 72-hour timeframe for rescue operations having elapsed.
“I understand that rescue operations are usually limited to 72 hours, but I firmly believe that God can perform miracles and enable us to save more of our people who are still trapped in the rubble,” she stated.
She added ; “I am instructing that the rescue operations must not stop. Extend the effort by an additional 24 hours to continue fighting for the lives of those who may still be alive.”
The rescue operations began immediately on Saturday when the building collapsed in the bustling business center.
Source: allafrica.com
Derick Junior (36), ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) anayekabiliwa na mashtaka mawili ya kujeruhi katika eneo la starehe la Club 1245, Masaki Dar es Salaam, leo Novemba 20, 2024 atasomewa hoja za awali za kesi inayomkabili.Continue Reading
Brasilia — President Samia expressed optimism that, with divine intervention, some victims might still be found alive beyond this period, despite the standard 72-hour timeframe
President Samia Suluhu Hassan has announced an additional 24 hours to rescue people trapped in a collapsed building at Kariakoo in Dar es Salaam.
In a statement issued on Tuesday by the Director of Presidential Communications, Ms Sharifa Nyanga, it was stated that the President gave the directive during a telephone conversation with Prime Minister Kassim Majaliwa regarding the ongoing rescue operation.
President Samia expressed optimism that, with divine intervention, some victims might still be found alive beyond this period, despite the standard 72-hour timeframe for rescue operations having elapsed.
“I understand that rescue operations are usually limited to 72 hours, but I firmly believe that God can perform miracles and enable us to save more of our people who are still trapped in the rubble,” she stated.
She added ; “I am instructing that the rescue operations must not stop. Extend the effort by an additional 24 hours to continue fighting for the lives of those who may still be alive.”
The rescue operations began immediately on Saturday when the building collapsed in the bustling business center.
President Samia also extended her heartfelt gratitude to the rescue teams and citizens working tirelessly to save lives, acknowledging their exceptional patriotism and commitment.
“To all the rescue teams and citizens tirelessly working to save lives, I send my heartfelt gratitude. Please let them know that their efforts are deeply appreciated. They are heroes of our nation, and I encourage them to keep fighting for our people,” she said.
The President urged families and the nation to remain patient, united, and prayerful, supporting the rescue teams as they work to save lives.
As of Monday, 16 people had been confirmed dead, while 86 had been rescued.
Source: allafrica.com
Zanzibar Investment News Tanzania Investors Ltd © 2025