Hop at last: Tanzania Breweries sells dormant Darbrew unit

By JAMES ANYANZWA

Tanzania Breweries Ltd (TBL) Plc has completed the sale of its entire 60 percent stake in the beer manufacturing subsidiary Darbrew Ltd and launched a facelift of its production facility at Kibo Breweries Ltd as part of a turnaround plan for the struggling dormant units.

The Dar es Salaam Stock Exchange-listed brewer approved the sale of Darbrew Ltd to a core shareholder Dar es Salaam City Council (DCC) on August 7, 2019, due to the non-performance of the subsidiary, but the conclusion of the deal has been delayed for years on undisclosed reasons. 

The company disclosed in its 2023 annual report that the transaction was completed during the accounting period ended December 31, 2023, as the beer maker moved to shore up its cash flow position amid a cocktail of domestic and global factors, including a significant increase in the cost of production and overheads as a result of the global supply chain disruptions caused by the conflict in the Middle East and eastern Europe. 

Locally, the company was impacted by the significant increase in excise duty on raw materials used in the production of beer, exceptionally wet weather and load shedding by the utility, Tanzania Electric Supply Company Ltd (Tanesco).

“During the year, management executed the Board’s approved disposal of the Darbrew Ltd made on August 7, 2019. The disposal involved offloading 60 percent of the Company’s investment in Darbrew Ltd to Dar es Salaam City Council (DCC), a core shareholder. The sale was executed on May 2, 2024, where the Sale Agreement, Transfer of Share Deeds and other documentations including formal handovers to the DCC were completed,” the company says.

“Decision was made due to non-performance of the Darbew Ltd in its business. Darbrew Ltd remained a dormant operation, and as of December 31, 2023, the subsidiary was held for sale (discontinued operations).”

Advertisement

Kibo upgrade

On the other hand, TBL’s management opted to upgrade the production facility at Kibo Breweries after the subsidiary remained dormant throughout the year, despite a Tsh42.41 billion ($15.83 million) investment.

“Kibo Breweries remained dormant throughout the year. Management continues to upgrade the production facility of the entity and it expects the malting plant to be completed in the year 2024,” the company says.

“During the year, management performed an impairment assessment of its investment in Kibo Breweries Limited. No impairment allowance was recognised.”

Kilimanjaro plant

In July 2023, the group announced its decision to invest and upgrade the Kilimanjaro Malting Plant after halting operations for six years — since 2017 — due to insufficient local barley grown in the area. 

High water usage and electricity costs as well as outdated technology consuming too many resources prevented the plant from restarting.

The plant is projected to process about 10,000 tonnes of barley in the initial phase and scale up to 28,000 tonnes of barley, contributing significantly to Tanzania’s agricultural economy and enhancing the welfare of the barley farming communities.

The initial phase of the project is expected to be operational by the fourth quarter of 2024.
“We are committed to empowering farmers through advanced agricultural techniques, business and financial literacy, which will in turn increase the value chain and benefit farmers who grow barley, sorghum and grapes,” the company says.

TBL stakes

Currently, TBL procures 74 percent of its raw materials from within the country.

TBL Plc is 63.95 percent owned by Anheuser-Busch InBev (AB InBev), the world’s largest brewer with operations in over 50 markets and a presence in 15 African countries.

The company’s principal activities are the production, distribution and sale of malt beer, non-alcoholic malt beverages and alcoholic fruit beverages in Tanzania, and exports to Nile Breweries Ltd and Zambia Breweries Ltd, all subsidiaries of AB InBev.

TBL has a controlling interest (65 percent) in a spirituous liquor company, Tanzania Distilleries Ltd, and 60 percent in Darbrew Ltd.
It fully owns Kibo Breweries Ltd.

In 2023 the group’s cash generated from operations declined by nine percent to Tsh335.86 billion ($125.42 million), from Tsh368.82 billion ($137.73 million) in 2022.

A total of Tsh87.53 billion ($32.68 million) was capital expenditure during the year, compared with Tsh82.35 billion ($30.75 million) invested in 2022.

“A capital investment plan is in place to ensure the optimal operation of all breweries and distilling plant. The Group and Company have set plans to ensure production, sales and market share are increased, maintained and sustained in the near future,” the company says.

Continue Reading

Tanzania: Tmx to Start Trading Cashew Nuts, Pigeon Peas This Season

Tanzania: Tmx to Start Trading Cashew Nuts, Pigeon Peas This Season

THE Tanzania Mercantile Exchange (TMX) announced on Tuesday that it will commence trading cashew nuts and pigeon peas this season, following a successful four-year trial period.

Mr. Prince Philemon, TMX’s Finance and Management Officer, told the ‘Daily News’ here on Tuesday that after conducting successful trials, the exchange will include these two crops starting from August.

“Following the introduction of sesame last month in Mtwara, cashew nuts and pigeon peas will now also be featured on the exchange,” Mr. Philemon stated.

During the sesame auction from last month to midthis month, a total of 27,550 tonnes were traded, amounting to a transaction value of 80bn/- .

The auctions, conducted across Mtwara, Masasi, and Nanyumbu under the Mtwara, Masasi, and Nanyumbu Agricultural Cooperative Union (MAMCU), showed increasing prices in each of the six sessions.

Sesame prices ranged from a high of 3,570/- per kilogramme to a low of 3,350/- per kilogramme, with the fifth auction averaging around 3,550/- per kilogramme.

“The TMX platform allows farmers to directly observe the entire bidding process, ensuring transparency and providing realtime market data,” Mr. Philemon added.

Initially, farmers were hesitant to use the platform due to concerns about potential fraud.

However, as they began selling their produce through TMX, they found it to be a reliable and transparent mechanism for pricing and selling their crops.

Encouraged by the success of sesame auctions, sesame farmers in Mtwara have urged the government to consider expanding the commodity exchange market to include other cash crops, aiming to maximize returns.

“At first, I was skeptical about TMX, thinking it might cheat us farmers. But we’ve realized it’s the best platform for us to benefit,” said Ally Omary, a sesame grower in Nanyumbu, Mtwara

Source: allafrica.com

Continue Reading

January, Nape: Ilianza kwa Magufuli sasa kwa Samia

Catherine Haddon, raia wa United Kingdom (UK), ni mtaalamu wa uendeshaji wa Serikali. Catherine aliwahi kusema: “Some reshuffles are planned well in advance and some are sudden but, they all have the potential to go off-course.”

Tafsiri yake ni kuwa; “baadhi ya mabadiliko ya baraza la mawaziri hupangiliwa vizuri mapema na mengine hutokea ghafla, lakini yote kwa namna moja au nyingine hufanana kwa Serikali kutoka nje ya mstari.” Yaani, mabadiliko yoyote ya baraza la mawaziri yana athari hasi kwa Serikali.

Nimeanza na nukuu ya Catherine, kuelekea kujenga tafakuri kufuatia Rais Samia Suluhu Hassan, kufanya mabadiliko mengine ya Baraza la Mawaziri. January Makamba, aliingia Baraza la Mawaziri la Rais Samia Septemba 2021, Agosti 2023, akawa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Hivi sasa January siyo waziri. Ametenguliwa.

Nape Nnauye, aliingia Baraza la Mawaziri la Rais Samia Januari 2022, akiwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari. Baada ya huduma yake ya miaka miwili na miezi sita iliyotimia, ametenguliwa. Nape siyo waziri tena. Hiyo ni kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu ya Julai 21, 2024.

Sura namba moja ya kuondoka kwa January na Nape kwenye Baraza la Mawaziri ni kuwa sasa, Rais Samia amejipangusa dhidi ya waliotengwa na mtangulizi wake, Dk John Magufuli. January na Nape, waliondolewa na Magufuli kwenye Baraza la Mawaziri katika nyakati za tamthiliya tata kisiasa.

Nape, alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuanzia Desemba 2015, aliondolewa na Magufuli Machi 23, 2017, baada ya kutofautiana mtazamo juu ya hatua zilizostahili dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Makonda, alituhumiwa kuvamia ofisi za Clouds Media Group (CMG), akiwa na askari wenye mitutu ya bunduki, kisha kulazimisha kurushwa hewani kwa maudhui yaliyokataliwa na uongozi wa Televisheni ya Clouds. Magufuli alitaka Makonda aachwe, Nape alisimama kidete kuhakikisha hatua zinachukuliwa. Akafukuzwa.

Nyakati za tamthiliya tata kisiasa, uliibuka mchezo wa kudukua mawasiliano ya watu, hasa wanasiasa. Sauti za Nape, January, Makamu Mwenyekiti CCM, Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana, Katibu Mkuu CCM mwaka 2006 mpaka 2011, Yusuf Makamba, Waziri wa Mambo ya Nje mwaka 2007 mpaka 2015, Bernard Membe, kwa nyakati tofauti walidukuliwa wakimteta Dk Magufuli.

Julai 21, 2019, Dk Magufuli alimweka pembeni January. Baadaye, Nape alionekana Ikulu, Dar es Salaam, ikaelezwa alikwenda kumwomba radhi Dk Magufuli.

Kisha, Dk Magufuli akatoka hadharani na kusema hata January alimwomba msamaha, akatangaza kuwasamehe wote. Pamoja na hivyo, baada ya Uchaguzi Mkuu 2020, Magufuli hakuwarudisha January na Nape kwenye Baraza la Mawaziri.

Hiyo ikaleta tafsiri kuwa January na Nape, walitengwa na Magufuli. Kitendo cha Rais Samia kuwarejesha Nape na January kwenye Baraza la Mawaziri, kilileta tafsiri ya watengwa wa Magufuli kukumbukwa na Mama (Rais Samia). Upo wakati ilielezwa kuwa “watengwa” ndio wenye zamu kwenye urais wa Mama. Mawaziri kadhaa kipindi cha Magufuli, waliwekwa kando. Sasa, watengwa wa Magufuli, wamekuwa watengwa wa Samia.

Kunani Wizara ya Mambo ya Nje?

Kila tafsiri inaweza kuwepo, swali moja litaendelea kutatiza wengi, ni kilichotokea ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Mapema, Julai 21, 2024, Ofisi ya Spika wa Bunge, ilieleza kupokea barua kutoka kwa aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mbarouk Nassor Mbarouk, kuomba kujiuzulu ubunge, kutokana na matatizo ya kijamii.

Katiba ya Tanzania, ibara ya 55 (4), inatoa sharti kwa Rais kuteua mawaziri na naibu mawaziri miongoni mwa wabunge tu. Kwa mantiki hiyo, kitendo cha Mbarouk kujiuzulu ubunge kilijenga tafsiri ya kujing’oa unaibu waziri.

Siku hiyo hiyo, usiku wake taarifa ya Ikulu ikatoka, ilieleza kumwengua January pamoja na Naibu Waziri mwingine wa Wizara ya Mambo ya Nje, Stephen Byabato. Kwa maana hiyo, bosi wa wizara na wasaidizi wake wawili, wote wameng’oka.

Mbarouk alisema, aliamua kujiuzulu kwa sababu ana matatizo ya kijamii. Taarifa ya Ikulu ikasema, Mbarouk atapangiwa kituo cha kazi. Mbarouk ni balozi. Maneno atapangiwa kituo cha kazi, yanaeleweka kuwa anarejeshwa kwenye uwanja wa diplomasia. Mbarouk alisema ana matatizo ya kijamii.

Je, akipangiwa kituo hayo matatizo ndiyo yataisha

Dhahiri, kuna jambo halipo sawa Wizara ya Mambo ya Nje. Rais Samia, ana wajibu wa kuueleza umma nini ambacho kimesababisha awaondoe mabosi watatu kwa mpigo, ingawa mmoja amesema atampangia kituo.

Rais Samia, alipoapa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Machi 19, 2021, alimteua Balozi Liberata Mulamula kuwa Waziri wa Mambo ya Nje. Mulamula aliapishwa Machi 31, 2021, lakini akaondolewa Oktoba 3, 2022. Akafuata Stergomena Tax, ambaye Agosti 31, 2023, alimpisha January, kisha yeye akahamia Wizara ya Ulinzi.

Kihistoria, Wizara ya Mambo ya Nje haina utamaduni wa mawaziri wake kubadilishwa mara kwa mara. Rais wa Tatu, Benjamin Mkapa, alidumu na Waziri wa Mambo ya Nje mmoja kwa miaka 10, ambaye ni Dk Jakaya Kikwete. Kisha, Rais wa Nne, Kikwete, aliteua mawaziri wawili ndani ya miaka 10.

Januari 4, 2006, Kikwete alimwapisha Dk Asha-Rose Migiro, kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Januari 11, 2007, Migiro aliteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Uteuzi huo wa Migiro UN, ulisababisha nafasi ya uwaziri ibaki wazi. Kikwete alimteua Bernard Membe, ambaye alidumu kipindi chote kilichokuwa kimesalia katika urais wake.

Rais wa Tano, Dk Magufuli, alidumu na mawaziri wawili wa Mambo ya Nje, kwa miaka yake mitano na siku 132, ambayo alihudumia nchi, kabla ya mauti kumkuta. Rais Samia, ndani ya miaka mitatu na miezi minne, ameshafikisha mawaziri wanne, Wizara ya Mambo ya Nje. Je, kunani? Sasa waziri ni Balozi Mahmoud Thabit Kombo.

Nape ni hadithi mbaya

Hivi karibuni, Nape akiwa ziarani mkoani Kagera, alinukuliwa akitoa matamshi tata. Nape aliwaambia wakazi wa Bukoba Mjini kuwa yeye ni mzoefu wa uchaguzi, na kwamba angemsaidia mbunge wao Byabato kushinda uchaguzi.

Akasisitiza kuwa yeye kama Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, anasimamia kampuni za simu, hivyo angezishawishi zitoe fedha kusaidia maendeleo jimboni kwa Byabato.

Watu wengi wameelekeza lawama zao kwenye kauli ya Nape kuwa angemsaidia Byabato kutangazwa mshindi hata nje ya sanduku la kura. Hata hivyo, kwangu kauli mbaya zaidi ni ile aliyosema kuwa angeshawishi kampuni za simu zipeleke maendeleo jimboni kwa Byabato, kitu ambacho hakina tafsiri tofauti ya rushwa.

Kiongozi wa Serikali anayepaswa kuwa msingi wa maadili kwenye eneo lake, hakupaswa kutoa kauli zenye ukakasi.

Waziri kutamba kuwa angeshawishi kampuni binafsi kuchangia maendeleo ili kumsaidia Byabato, inajenga wasiwasi kuwa pengine ndiyo ulikuwa mchezo wake.

Tena kwa masilahi binafsi. Waziri badala ya kusimamia sheria na sera, kuhakikisha kampuni zinatoa huduma bora, yeye anawaza kuzishawishi zimchangie pesa.

Hii ni hadithi mbaya ya Nape.

Maswali ni mengi

Kutoka Nape hadi January, sasa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ni Jerry Silaa, aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Deogratius Ndejembi, ndiye anakuwa Waziri wa Ardhi, akitokea Wizara ya Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu. Ndejembi amempisha Ridhiwani Kikwete.

Pitia mabadiliko yote, jambo moja hatuwezi kubishana ni kuwa Baraza la Mawaziri chini ya Rais Samia, limekuwa na mabadiliko ya mara kwa mara bila kuwa na maelezo ni kwa nini yanatokea.

Ndani ya miaka mitatu ya Rais Samia, ukimwondoa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, mawaziri waliobaki wote walishafanyiwa mabadiliko.

Yupo mtu anaweza kulileta jina la Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, kuwa hajabadilishwa. Awali, wizara ilikuwa ikiitwa Fedha na Mipango, kisha ikagawanywa mara mbili. Mwigulu amebaki kuwa Waziri wa Fedha. Mipango ikaanzishiwa wizara mpya ya Uwekezaji na Mipango, ambayo waziri wake ni Profesa Kitila Mkumbo.

Mabadiliko ya mara kwa mara yanaleta maswali, je, mawaziri hawawezi kazi au hulka zao hazimfurahishi Rais Samia, kwa hiyo anawabadilisha kila baada ya miezi?

Je, ndani ya Serikali kuna usaliti mkubwa, ndiyo sababu hataki kutulia na wasaidizi wake kwa muda mrefu?

Katika historia, Tanzania chini ya Rais Samia imeweka rekodi ya kubadili wakurugenzi wakuu wanne wa Idara ya Usalama wa Taifa, ndani ya miaka mitatu.

Januari 2023, alimwondoa ofisini aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Diwani Athuman. Aliyempokea Diwani ni Said Massor.

Miezi saba ilitosha kwa Massor kufika tamati Tiss. Agosti 28, 2023, Balozi Ally Siwa, aliapishwa kuwa DGIS. Kisha, ilipofika Julai 11, 2024, Rais Samia alimwapisha Suleiman Abubakar Mombo kuwa Mkurugenzi Mkuu mpya wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Kwa nini Serikali ya Rais Samia haitulii? Wapo watu wanadai shida kubwa ni Uchaguzi Mkuu 2025.

January ametajwa mara nyingi kuwa na mipango ya kuwania urais mwaka 2025. January mwenyewe alishajitokeza na kueleza kumuunga mkono Rais Samia. Je, ni mapambano dhidi ya adui asiyekuwepo?

Mabadiliko yafanyike. Iwe kwa nia njema ya kuhudumia nchi au hofu na visasi vya kutoaminiana, muhimu ibaki kichwani kwamba Serikali inapaswa kuonekana imetulia, ikitekeleza wajibu wake kwa wananchi.

Panga pangua ya mawaziri hadi wakurugenzi Tiss, ni kiashiria cha Serikali kutotulia. Zaidi, ni kama alivyosema Haddon, hakuna mabadiliko ya Baraza la Mawaziri ambayo hayaipeleki Serikali nje ya mstari.

Kuondolewa kwa mawaziri wawili, January Makamba, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Nape Nnauye, aliyekuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, kumeibua mjadala, hasa mitandaoni.

Wananchi wamekuwa na maoni tofauti kuhusu kuondolewa kwa mawaziri hao, huku wengi wakihusisha kuondolewa kwa Makamba na mbio za urais, huku wengine wakieleza kwamba Nape amejimaliza mwenyewe kwa kauli yake aliyoitoa hivi karibuni.

Akizungumzia uamuzi wa kuondolewa kwa Nape, Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk Revocatus Kabobe alisema pengine kauli yake ya Julai 15 ndiyo iliyomponza.

“Yalikuwa makosa makubwa kwa kiongozi mwandamizi kama Nape kutoa kauli kama hizo zenye kukichafua chama (CCM) na Serikali juu ya uchaguzi.

“Kauli yake inaweza kuwa imechukuliwa kama uthibitisho kwa wapinzani ambao mara zote wamekuwa wakilalamika kuibiwa kura,” ameeleza.

Dk Kabobe amehusisha kuondolewa kwa Nape na madai yaliyowahi kutolewa na mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde akimtuhumu kwa hujuma za uchaguzi ndani ya CCM wakati wanapiga kura za kuwachagua wabunge wa Afrika Mashariki.Continue Reading

Tanzania: Over 33,900 Shortlisted for Police Force Vacancies

Tanzania: Over 33,900 Shortlisted for Police Force Vacancies

A total of 33,998 candidates have been shortlisted for various vacancies announced by the Tanzania Police Force.

Of the shortlisted candidates, 31,930 are from Tanzania Mainland and 2,068 from Zanzibar.

According to information published on the Police Force website and shared on the Force’s official social media platforms on Monday, the interviews will be conducted over 14 days, from July 29 to August 11, 2024.

The list, seen by the Daily News Digital, shows that Dodoma Region is leading with 3,051 applicants who have completed Form Four and Form Six, followed by Arusha (2,957), Mwanza (1,948), Temeke (1,577), and Kilimanjaro (1,426).

Areas with the fewest candidates are Rufiji (134), Tarime (127), and Songwe (374).

ALSO READ: TIOB addresses youth unemployment

In the Mainland, the list shows that 2,238 out of 31,930 candidates hold degrees, diplomas, and certificates, while 29,692 are Form Four and Form Six leavers.

In Zanzibar, 739 out of 2,068 candidates hold degrees, diplomas, and certificates, while 1,329 are Form Four and Form Six leavers.

The statement added that interviews for degree, diploma, and certificate holders will be conducted at the Police Academy (DPA) in Dar es Salaam, while those who hold Form Six and Form Four certificates will remain in their respective regions.

In Zanzibar, candidates from Unguja will be interviewed at the Police Headquarters in Zanzibar, while those who applied from Pemba will be interviewed at the South Pemba Regional Police Commander’s offices.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Wadau waonyesha kasoro ulaji mbogamboga, matunda

Dar es Salaam. Wakati ulaji wa mbogamboga na matunda ukitajwa kuwa moja ya njia ya kujenga mwili wa binadamu na kumuepusha na magonjwa, imeelezwa mboga nyingi zinazozalishwa hazifai kwa ajili ya matumizi ya binadamu.

Hiyo ni kutokana na kuwa na bakteria wanaoweza kuathiri matumbo ya watu na viuatilifu vilivyozidi kiwango.

Hayo yamesemwa leo Jumatatu, Julai 22, 2024 katika mjadala wa X Space ulioandaliwa na Mwananchi kwa kushirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) pamoja na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) wenye mada inayosema: ‘Mambo muhimu ya kuzingatia katika uandaaji, ulaji wa mbogamboga na matunda.’

Akizungumza katika mjadala huo, Mtaalamu wa Kituo cha Mbogamboga duniani, Jeremiah Sigalla amesema kupitia ukaguzi waliofanya waligundua baadhi ya mboga katika masoko ya Arusha na Dar es Salaam zilikuwa chafu na zinahatarisha afya ya mlaji.

Mtaalamu huyo amesema katika taasisi yao ya World Vegetable Centre kupitia tafiti walizozifanya wamegundua mboga hizo zina kiwango kikubwa cha wadudu wanaodhuru tumbo.

“Kupitia kuangalia viambata ambavyo vinaathiri lishe na afya ya mlaji, mboga hizi zimekuwa na kiwango kikubwa cha bakteria wanaodhuru mazingira ya tumbo na katika baadhi ya masoko ya Arusha ya Dar es Salaam tumekuta mboga nyingi ambazo zinaonekana nzuri kwa macho ukazinunua, lakini kwa afya si salama,” amesema Jeremiah.

Amesema kwa kuwa maeneo mengi ya mijini mboga hizo zinahitajika kwa wingi, ndio maana hata mazingira ya uzalishaji wake si salama.

Hivyo amesema kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kama FAO wanaona ni muhimu elimu kutolewa kwa wakulima katika matumizi ya dawa ambazo zinatumika kuzitunza mboga hizo.

“Kuna baadhi ya dawa na mbolea maarufu kama busta zinachangia uharabifu wa hizi mboga. Teknolojia inakua, lakini njia za teknolojia hiyo kama mzalishaji asipopata taarifa sahihi itaathiri uzalishaji na tija inayopatikana katika uzalishaji wake,” amebainisha Sigalla.

Katika hilo, Mtafiti na mtaalamu wa chakula, Martin Kimanya amesema mtu anapokula mbogamboga zilizochafuliwa ikiwemo kemikali ni sawa na kutokuwa navyo nyumbani.

“Tatizo kubwa lililopo nchini katika eneo la mbogamboga ni uchafuzi kutokana na matumizi ya viuatilifu katika kiwango ambacho si bora,” amesema.

Amesema kuwa pia kuna wakulima wanataka kuongeza uzalishaji, lakini wamekuwa wakifanya katika namna ambayo haifai na wengi hawana ufahamu ambao utawafanya wajue ni aina gani ya viuatilifu si sahihi vya kutumia.

“Kwa bahati mbaya udhibiti wa viatilifu vilivyopo sokoni kwetu pia si mzuri, kwani baadhi vinaweza kuwa vimepigwa marufuku huko nje, lakini bado vikawepo sokoni huku wakulima wakikosa mbinu sahihi ya kutumia viatifu hivyo,” amesema Profesa Kimanya.

Amesema ukubwa wa hili tatizo unatokana na mambo matatu la kwanza ni wakulima kutumia viatifu ambavyo baadhi haviruhusiwi na hawajui namna nzuri ya kuvitumia, maofisa ugani na kilimo kutokuwa na uwezo wa kumfikia mtu kwa namna inayotakiwa ili kumueleza namna nzuri ya utumiaji ili kutoathiri afya ya mlaji.

Alichokisema Malembo

Kuhusu maofisa ugani kuhudumia wakulima, Mkurugenzi wa Malembo Farm, Lucas Malembo amesema utafiti uliofanywa na Jukwaa Huru la Kilimo ANSAF mwaka 2017 umeonyesha asilimia 48 ya vijiji 15,082 vilivyosajiliwa nchini havina maofisa ugani wa kutosha.

Utafiti unaonyesha pengo hilo wakati ambao sera ya kilimo ya mwaka 2013 ikitaka kila kijiji kuwa na afisa ugani mmoja.

“Katika hali ya kawaida bado kuna changamoto ya usalama wa mboga tunazokula kutokana na uhaba wa watalaamu. Matumizi mabaya ya viuatilifu ni matokeo ya wakulima wengi kutokuwa na elimu ya kilimo biashara sensa ya kilimo ya mwaka 2019/2020 inaonyesha matumizi ya viuatilifu ni asilimia mbili ya wakulima wote nchini,” amesema.

Hata hivyo, Profesa Kimanya amesema kutokana na kutokuwa na uhakika na usalama wa tunda linapotoka ni vyema kuliosha na kulimenya kabla ya kuanza kula.

Kuosha na kumenya kunapunguza kemikali ambazo zinapatikana, ijapokuwa utapunguza baadhi ya virutubisho katika tunda hilo.

Faida za tunda

Pamoja na changamoto hizo, Mkurugenzi Idara ya Elimu na Mafunzo ya Lishe kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC,) Dk Esther Nkuba amesema mwili wa binadamu unahitaji virutubisho zaidi ya 50 kwa siku na kila chakula kina virutubisho zaidi ya kimoja, hivyo ulaji wa matunda wakati wa kula iwe asubuhi mchana au jioni hauna tatizo.

“Hakuna tafiti inayosema ukila matunda kwa kuchanganya inatengeneza sumu. Ukila ndizi ukachanganya na parachichi mwili wenyewe unajua chakufanya,” amesema Dk Nkuba.

Akichangia hoja hiyo, Mkurugenzi wa Hospitali ya Muhimbili, Profesa Mohammed Janabi amependekeza watu kupenda kula matunda yenyewe badala ya kunywa juisi, ili kupunguza wingi wa sukari anayoweza kuinywa kwa wakati mmoja.

“Pia watu wale vyakula badala ya kutumia dawa za virutubishi, kwani haviwezi kuwa mbadala wake,” amesema Profesa Janabi.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Zanziba, Dk Omar Ally Amir amesema katika kukabiliana na changamoto hizo wanachokifanya sasa ni kuangalia namna wanayoweza kuwafikia wakulima, ili kuzalisha mbogamboga na matunda ambayo ni salama kwa walaji.

“Pia tunajaribu kuhimiza kilimo hai kisichotumia viuatilifu, ili mazao yanapozalishwa yawe salama kwa watumiaji,” amesema Dk Amir.Continue Reading

Tanzania’s President Samia Suluhu fires foreign, information ministers

By REUTERS

Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has fired two senior members of government including the foreign minister in a mini-cabinet reshuffle, her office said.

The changes came as Hassan seeks to regain trust from foreign powers over a programme of economic and political reforms, including easing restrictions on opposition parties and media, that some critics had seen as faltering.

The presidency announced late on Sunday, July 21, that Hassan terminated the appointments of the minister of foreign affairs and East Africa cooperation, January Makamba, and the minister of information, communication and information technology, Nape Nnauye.

They are influential figures in the ruling party, Chama cha Mapinduzi (CCM).

No reason was given for their removal. Makamba and Nnauye did not immediately respond to requests for comment.

Read: Samia replaces TRA chief amid diplomats, traders tax complaints

Advertisement

The dismissal of Nnauye comes a week after comments he made surfaced in a video, saying elections results would depend on who counts votes and announces the results.

Nnauye later apologised, saying it was a joke, but activists and some social media users said the statement undermined Hassan’s push to improve democracy.

Also read: Will sacked minister Nnauye join rebellion in CCM?

Hassan appointed Mahmoud Thabit Kombo as new foreign affairs minister and Jerry Silaa as minister of information, communication and information technology.

Before Kombo’s appointment, he was Tanzania’s ambassador to Italy while Silaa was the minister of lands, housing and human settlements development. Two more ministers and deputy ministers were also appointed, the presidency said.

In power since 2021, Hassan’s government has won praise for rolling back her predecessor’s crackdowns on the opposition and civil rights groups. But arrests last year of a lawyer and an opposition politician have raised questions over her government’s human rights record.

Continue Reading

Rais Samia asimulia machungu mpunga wake ulivyoliwa na mifugo

Dodoma. Rais Samia Suluhu Hassan ameelezea machungu wanayokutana wakulima kwa mazao yao kuliwa na mifugo, huku akasimulia majibu ya dharau aliyopewa na mfugaji baada ya mifugo kula mpunga katika shamba lake, eneo la Dutumi, Mkoa wa Morogoro.

Akizungumza leo Julai 20, 2024 wakati akizungumza na machifu nchini, Rais Samia amesema kuna migogoro kati ya wakulima na wafugaji ambapo watu wamekuwa wakipigwa, kuuana na mazao yao kuliwa na mifugo.

“Niwaombe sana machifu wenzangu tukayasimamie haya. Tunapoacha wakulima na wafugaji wakauana na mara nyingi wanaoonewa ni wakulima, hii si haki. Nitakupeni mfano ulionipata mimi mwenyewe,” amesema.

Amesema aliwahi kulima mpunga katika eneo la Dutumi, Mkoa wa Morogoro na kwamba alilima mara ya kwanza kwa kuweka fedha yake yote kwenye shamba hilo.

“Basi wakaja watu na ng’ombe wao, mpunga umenawiri, nishasema hapa umasikini bye bye (kwa heri), dakika 10 nyingi mpunga wote ukaingia ng’ombe kama 300, wakaula. Sikuweza kufanya kitu chochote,” amesema.

Hata hivyo, amesema watoto wake walimweleza kuwa wajaribu tena kulima kwenye shamba hilo na hivyo akaamua kulima nusu ya eneo alilolima awali.

Amesema lakini mpunga ulivyoanza kuchanua na kuvutia na ukaanza kutoa harufu, ng’ombe waliingia tena katika shamba na kuula tena.

“Tulipokwenda katika kesi, mara hii nikasema hapana. Nikachukua mtendaji wa kijiji, polisi, sijui nani nikasema twende. Tulipokwenda katika kesi mfugaji anasema ng’ombe wangu kala mpunga wapi? Aliingia katika ghala ya nani, amekula majani tu,” amesema.

Rais Samia amesema inapotokea dharau ya namna hiyo ambayo inatolewa kwa mtu ambaye ameshapoteza nguvu na fedha na jasho, haileti amani Tanzania.

“Mfugaji anasema ng’ombe amekula majani tu, hajaingia katika ghala kula mpunga wa mtu. Sasa mambo kama haya yakitokea hayaleti amani Tanzania. Niwaombe sana machifu katika maeneo yetu tukayasimamie hayo,”amesema.

Aidha, Rais Samia amewataka Watanzania, viongozi wa Serikali, taasisi zisizo za kiserikali, viongozi wa kidini na machifu, kukemea vitendo viovu vinavyokiuka maadili ya Kitanzania.

“Tunapoona vitendo vya ovyo katika maeneo yetu, machifu tusemeni, tukemee. Kama mnamuona mkuu wenu wa wilaya hafanyi vyema mkemeeni, msemeni, muumbueni tumjue. Kama mnamuona kiongozi haendi mwendo mwema tuambieni tumjue ili tulete viongozi waadilifu na mambo yaende vizuri,” amesema.

Amesema mwongozo kwa ajili ya kuratibu shughuli za machifu nchini unaandaliwa, ambao ndio utaweka utaratibu wa kuwasema viongozi wanaokiuka maadili na sio kusimama na kuropoka.

“Niwaombe twende tukakemee vitendo viovu vinavyokiuka maadili yetu. Tudumishe upendo, amani, utu na kuheshimiana,” amesema.

Pia amewataka Watanzania wanapohama kutoka eneo moja kwenda jingine, kufuata mwongozo unaowataka kuchukua barua wanapotoka na kupeleka wanakokwenda ili kuwatambulisha.

“Lakini watu wanahamishana usiku na malori, wao na wanyama, wakifika mahali wanateremshana, pengine kuna mwenyeji anawasubiri wanavamia mapori, wanavamia misitu wanaingia huko,wengine wanafyeka mapori,” amesema.

Naye, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro amesema kwa sasa Serikali iko katika hatua za mwisho ya kuandaa mwongozo wa kutambua machifu na viongozi wa kimila, ili waweze kupata heshima wanayostahili kwa jamii na Serikali kwa ujumla.

“Mwongozo unaoandaliwa utatambua machifu na viongozi wa kimila katika ngazi ya wilaya na mikoa ili kutoa fursa kwa machifu kutekeleza jukumu lao la msingi la kuwawezesha Watanzania kuendelea kupata haki yao ya kikatiba na uhuru wa kuabudu kupitia mila, desturi na imani za kijadi,” amesema.

Aidha, Dk Ndumbaro amesema taarifa za uchumi za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), mwaka 2023 zinaonyesha kuwa sekta ya utamaduni na sanaa inaongoza kwa kukua nchini ambapo imekuwa kwa asilimia 17.7.

Awali, Mwenyekiti wa Umoja wa machifu wa Tanzania, (UMT), Antonia Shangalai amesema kuwa Rais Samia amepandisha hadhi ya wanawake wa Tanzania kwa kuwapandisha vya kutosha na kuwataka mawaziri kutoa ushirikiano wa kutosha kwake.

“Sisi machifu tuko nyuma yenu tutaenzi mila, kuheshimiana, kuwaheshimu wakubwa na mambo yote yanayokwenda na mila na desturi zetu tusiyoyataka na nyie hamyataki na Serikali haiyataki. Tunaendelea kupambania hayo yasiendelee kuwepo kabisa,”amesema.

Akitoa baraka za machifu, Chifu Rocket Mwashinga amesema wakati nchi inaelekea kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu, anahimiza Watanzania kulinda amani ya nchi na kuonya suala la ukabila.Continue Reading