Balozi Sefue aalika mawazo kuboresha makusanyo ya kodi

Moshi. Tume ya Rais ya Maboresho ya Mifumo na Muundo wa Kodi imewataka Watanzania kuwasilisha mawazo ya namna Serikali inavyoweza kuongeza ukusanyaji wa mapato bila kuathiri mazingira ya biashara, hatua itakayochochea ukuaji wa maendeleo.

Rai hiyo imetolewa leo, Jumatano, Januari 29, 2025, na Mwenyekiti wa tume hiyo, Balozi Ombeni Sefue, wakati wa mkutano wa majadiliano ya wadau wa kodi mkoani Kilimanjaro, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Moshi. Mkutano huo pia ulilenga kukusanya maoni na mapendekezo ya maboresho ya kodi.

Balozi Sefue amesema wigo wa ulipaji kodi nchini bado ni mdogo, huku wastani unaotakiwa kwa nchi za Afrika zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara ukiwa asilimia 15 – 16, wakati Tanzania ikiwa katika asilimia 11.9, hivyo bado kuna kazi kubwa ya kuongeza makusanyo ya kodi.

Amesema kwa sasa kuna dirisha la wiki mbili, hivyo ametoa rai kwa wananchi wa Kilimanjaro na Tanzania kwa ujumla kuwasilisha mawazo yao kwa njia ya maandishi kuhusu namna ambavyo serikali inaweza kuongeza makusanyo ya kodi kwa kufuata misingi ya haki.

“Tuna kazi kubwa ya kuongeza makusanyo ya kodi kwa upande mmoja, lakini kwa upande mwingine, tunakusanyaje mapato kwa kuzingatia misingi ya kodi inayotambulika kimataifa

“Msingi mmoja ni haki, kwamba nchi isiendeshwe kwa kodi za watu wachache—kila mwenye kipato alipe kwa kadri ya kipato chake, lakini alipe kwa namna inayotenda haki, yaani haki ionekane katika kukadiria kodi inayotakiwa kulipwa na haki ya mtu ya kusikilizwa malalamiko yake,” amesema Sefue.

Ameongeza kuwa, “Natoa wito kwa Watanzania wote popote walipo, kama una wazo zuri la namna gani tunaweza kuongeza kodi lakini kwa njia ambayo haitaathiri mazingira ya biashara, tafadhali tumia fursa hii kuwasilisha. Tuna dirisha la wiki mbili, tumia mifumo iliyowekwa ya kuwasilisha maoni.”

Changamoto za wafanyabiashara

Wakizungumza katika mkutano huo, baadhi ya wafanyabiashara na wadau kutoka sekta mbalimbali mkoani Kilimanjaro walikosoa baadhi ya mifumo ya ukusanyaji kodi, ikiwemo wa ukaguzi wa mahesabu ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ambao wamedai unawaumiza.

Jonathan Christopher, amesema ili kurahisisha ulipaji wa kodi na kuwawezesha wafanyabiashara kulipa kwa wakati, ipo haja ya TRA kuwekewa ukomo wa kufanya ukaguzi wa mahesabu ili kuondoa usumbufu.

“Tunawasilisha mahesabu TRA ndani ya muda uliowekwa, lakini baada ya kuyapokea, TRA inaweza kuchukua hadi miaka mitano kabla ya kuyapitia. Wanapoyakagua kwa wakati mmoja, mfanyabiashara anaweza kufanyiwa ukaguzi wa miaka mitatu hadi minne.

“Katika ukaguzi huo, mbali na kodi aliyopaswa kulipa, anaweza pia kutozwa adhabu kwa makosa ya nyuma ya miaka mitatu hadi minne, jambo ambalo ni mzigo kwa wafanyabiashara,” amesema Christopher.

Rajabu Msangi, amesema kumekuwa na changamoto katika ukadiriaji wa kodi, ambapo wakati mwingine husababishwa na baadhi ya wafanyakazi wa TRA wasio waaminifu, jambo ambalo huwaumiza wafanyabiashara.

“Kodi ni kwa maendeleo ya nchi na ni lazima kila mmoja apambane kutimiza malengo ya Serikali, lakini changamoto huwa inajitokeza wakati wa ukadiriaji wa mapato. Mfano, unakuta mtaji wako ni Sh10 milioni, unakuja kupigiwa kodi ya miaka mitano Sh20 milioni ilihali mtaji wako haufikii hapo. Hii ni changamoto kubwa.

“Tunaamini maoni tuliyotoa yatafanyiwa kazi na watakuja na mrejesho ambao utakuwa ni mstakabali mzuri kwa maendeleo ya nchi yetu,” amesema Msangi.

Kwa upande wake, Ibrahim Shayo amependekeza maboresho ya kodi ya huduma na kuomba wafanyabiashara kulipa kodi kutokana na faida waliyozalisha.

“Lipo suala la kodi ya huduma, tunatambua kodi hii ni takwa la kisheria, lakini tumekuwa tukitozwa kodi kutokana na mitaji tuliyo nayo, ambayo wengi ni mikopo ya benki. Tunaomba kodi hii ikafanyiwe maboresho na tukalipe kodi inayotokana na kile tunachozalisha,” amesema Shayo.

Katika hatua nyingine, Shayo amependekeza upanuzi wa barabara ya Tanga-Moshi na kupanua njia hadi nne ili kurahisisha usafiri na usafirishaji, hasa katika kipindi hiki ambacho kumekuwa na ongezeko la mizigo inayosafirishwa kupitia Bandari ya Tanga.

“Naomba tuangalie hili la barabara. Kuna mikoa ambayo iko karibu na bandari, mfano sisi Kilimanjaro tupo karibu na Bandari ya Tanga, lakini barabara ya kutoka Tanga-Moshi kwa sasa imejaa malori na ni nyembamba. Ifike mahali turekebishe sheria na tujenge barabara za njia nne hadi sita. Hii pia itapunguza ajali na kuwezesha usafiri salama,” amesema Shayo.

Akizungumzia suala la upanuzi wa barabara hiyo, Balozi Sefue amesema ni wazo zuri, lakini akasisitiza ulipaji wa kodi.

“Wazo lako la kupanua barabara hii nalikubali kabisa, sasa tuongeze mapato ya serikali ili tuweze kujenga barabara,” amesema Balozi Sefue.

Oktoba 4, 2024, Rais Samia Suluhu Hassan alizindua tume hiyo kwa lengo la kuboresha ukusanyaji wa kodi, kuhakikisha ufanisi katika matumizi yake, pamoja na kushughulikia changamoto zinazoathiri mfumo wa kodi nchini.Continue Reading

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit

Dar es Salaam — Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has declared an outbreak of Marburg virus, confirming a single case in the northwestern region of Kagera after a meeting with WHO director-general Tedros Adhanom Ghebreyesus.

The confirmation follows days of speculation about a possible outbreak in the region, after the WHO reported a number of deaths suspected to be linked to the highly infectious disease.

While Tanzania’s Ministry of Health declared last week that all suspected cases had tested negative for Marburg, the WHO called for additional testing at international reference laboratories.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”Amelia Clemence, public health researcher

Subsequent laboratory tests conducted at Kagera’s Kabaile Mobile Laboratory and confirmed in Dar es Salaam identified one positive case, while 25 other suspected cases tested negative, the president told a press conference in Dodoma, in the east of the country today (Monday).

“The epicentre has now shifted to Biharamulo district of Kagera,” she told the press conference, distinguishing this outbreak from the previous one centred in Bukoba district.

Tedros said the WHO would release US$3 million from its emergencies contingency fund to support efforts to contain the outbreak.

Health authorities stepped up surveillance and deployed emergency response teams after the WHO raised the alarm about nine suspected cases in the region, including eight deaths.

The suspected cases displayed symptoms consistent with Marburg infection, including headache, high fever, diarrhoea, and haemorrhagic complications, according to the WHO’s alert to member countries on 14 January. The organisation noted a case fatality rate of 89 per cent among the suspected cases.

“We appreciate the swift attention accorded by the WHO,” Hassan said.

She said her administration immediately investigated the WHO’s alert.

“The government took several measures, including the investigation of suspected individuals and the deployment of emergency response teams,” she added.

Cross-border transmission

The emergence of this case in a region that experienced Tanzania’s first-ever Marburg outbreak in March 2023 has raised concerns about cross-border transmission, particularly following Rwanda’s recent outbreak that infected 66 people and killed 15 before being declared over in December 2024.

The situation is particularly critical given Kagera’s position as a transport hub connecting four East African nations.

Amelia Clemence, a public health researcher working in the region, says constant vigilance is required.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”

The Kagera region’s ecosystem, home to fruit bats that serve as natural reservoirs for the Marburg virus, adds another layer of complexity to disease surveillance efforts.

The virus, closely related to Ebola, spreads through contact with bodily fluids and can cause severe haemorrhagic fever.

Transparency urged

Elizabeth Sanga, shadow minister of health for Tanzania’s ACT Wazalendo opposition party, says greater transparency would help guide public health measures.

“This could have helped to guide those who are traveling to the affected region to be more vigilant and prevent the risk of further spread,” she said.

WHO regional director for Africa Matshidiso Moeti says early notification of investigation outcomes is important.

“We stand ready to support the government in its efforts to investigate and ensure that measures are in place for an effective and rapid response,” she said, noting that existing national capacities built from previous health emergencies could be quickly mobilised.

The situation coincides with leadership changes in Tanzania’s Ministry of Health, with both the chief medical officer and permanent secretary being replaced.

This piece was produced by SciDev.Net’s Sub-Saharan Africa English desk.

Source: allafrica.com

Continue Reading