Anayedaiwa kuchukuliwa na askari kwa mahojiano akutwa ameuawa Zanzibar

Anayedaiwa kuchukuliwa na askari kwa mahojiano akutwa ameuawa Zanzibar

Anayedaiwa kuchukuliwa na askari kwa mahojiano akutwa ameuawa Zanzibar

“Mwanangu ameuawa, kifo cha kikatili naomba haki itendeke waliofanya hivi wachunguzwe, ni kweli kifo kipo lakini sio cha namna hii…”

Hii ni kauli ya Saada Ramadhan Mwendwa mama mzazi wa Ramadhan Idd Shaaban (48) akianza kusimulia jinsi mwanaye alivyochukuliwa na watu waliojitambulisha ni askari wakidai wanakwenda kufanya mahojiano naye lakini aliokotwa akiwa amefariki dunia eneo la Mbuzini Kijichi Unguja.

Kwa kipindi cha hivi karibuni matukio ya watu kutekwa, kupigwa, kuumizwa na kuuawa yameshika kasi.

Kwa tukio la karibuni zaidi ni lile la Mjumbe wa Sekretarieti ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Ali Kibao ambaye alichukuliwa kwenye gari Septemba 6, 2024 akitoka Dar es Salaam kwenda Tanga na mwili wake uliokotwa Ununio uso wake ukiwa umeharibika kiasi cha kutotambulika.

Akisumulia mama huyo huku akitokwa na machozi, Saada ametumia fursa hiyo kumuomba Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama kuchunguza tukio hilo na waliofanya hivyo wachukuliwe hatua.

Akisimulia mkasa huo nyumbani kwake Chumbuni Oktoba 2, 2024 Saada amesema mwanaye alichukuliwa Septemba 24, 2024 saa 12:00 jioni lakini mwili wake uliokotwa kesho yake Septemba 25 ukiwa umeunguzwa, jicho moja limetobolewa na ulimi umetoka nje ambapo uchunguzi wa polisi ulieleza kuwa ameuawa.

“Siku hiyo mwanangu alikwenda kutembea jioni eneo la Amani Baa, saa 12:00 za jioni walikuja vijana watano wakamfuata alipokuwa amekaa na kumuita kwa jina wakasema wana shida naye waende nje wakazungumze wakidai wao ni askari na wana RB wanamtafuta,. 

“Walipanda naye kwenye gari wakamwambia wanampeleka polisi Mwanakwerekwe lakini walipofika walipitiliza. Saada anasema mwanaye alikuwa na rafiki yake ambaye aliongozana naye kwenda kituo cha polisi ila baada ya kupitiliza alipohoji mbona wamepita walimshusha.

“Walichokifanya ndio hicho kilichotokea, wamempiga mwanangu wamemuunguza moto kwa shoti za umeme na kumtoboa jicho moja la kulia,” amesimulia akieleza kifo cha mwanaye wa kwanza ambaye ameacha mjane na watoto wanne.

Anasema usiku wa siku hiyo mke wake Shaaban alipiga simu baada ya kuona mumewe hajarejea lakini kuna mtu alipokea simu hiyo akasema asiwe na wasiwasi bado anahojiwa na askari akimaliza atarejea nyumbani.

Baada ya kuambiwa hivyo, alitulia lakini kadri muda ilivyoendelea akawa anaingiwa zaidi na wasiwawasi ndipo alinipigia mimi simu akisema kuna muda alimpigia askari wakasema bado wapo naye lakini mpaka sasa hajarejea.

“Baadaye mimi nilipiga simu ikawa haipatikani nikaanza kumtumia meseji, mwanangu upo wapi mbona hujarudi baba, simu haipatikani nikajua ujumbe unaingia kumbe matokeo yake wameshampiga na kumfanyia ukatili huo,” amesema.

Amesema walipoamka asubuhi Septemba 25 walienda kutoa taarifa katika vituo vitatu vya polisi.

Hata hivyo, amesema anashukuru polisi kwani walionesha jitihada za kupiga simu katika vituo vingi kuulizia iwapo kuna mtu wa namna hiyo lakini majibu yalikuwa hapana.

Akiendelea kusimulia, Saada amesema ulipofika mchana alipigiwa simu na mwanawe mkubwa kuwa kuna maiti imeokotwa katika njia ya Mbuzini Kijichi akiwa na vitambulisho na limeonekana kuna jina la Ramadhani Iddi na walipokwenda katika chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Mnazi Mmoja wakakuta ni yeye.

“Mdomo ulikuwa wazi, jicho limetumbuliwa na mwili wote umechomwa chomwa, ila niliwaambia wanangu tufanye utaratibu kuchukua maiti,” amesema.

“Kwa kweli kilichotokea kwa mwanangu naomba sana, serikali yangu ni sikivu ya Zanzibar na inatupenda wananchi wanyonge, kwa hili nataka isikie kilio changu waliofanya ukatili huu aliyefanya ukatili huu wapatikane haki itendeke,” amesema na kuongeza.

“Mwanagu kaonewa…, kapata mateso ndani ya nafsi yake, kwasababu unapotiwa moto kila mtu anajua, kama ni kifo kila mtu atakufa lakini sio kwa kifo kile, naomba serikali ichukue hatua haina uonevu watu wote ni watu wake, tumeumia familia hatuna pa kulilia serikai ina mkono mrefu itawapata waliofanya kitendo hiki sheria ni kwa watu wote,” amesisitiza.

Saada amesema ameshakuwa na woga hata kwa watoto wake wengine kwasababu hajui kilichofanywa mwanaye kuuawa.

“Sasa sijui kama litaishia kwa Ramadhan au mimi mwenyewe au watoto wangu wengine hadi wajukuu zangu wangu kwakweli tunakosa amani.”

Mama mdogo wa marehemu, Yunes Kitarao amesema jambo hilo lnawasikitisha na kuwaumiza kwanini auawe kwa ukatili wa namna ile.

“Kwanini mtu atekwe, anaambiwa anachukuliwa na askari na wanasema yupo katika mikono salama watamrudisha na kwanini hakurudishwa akiwa mzima, dhamira hiyo imeniumiza sana, mtoto wa dada yangu, sijawahi kusikia amegombana wala kutukana na mtu,” amesema Yunes.

Amesema mambo hayo yamekuwa yakitendeka maeneo mengine sasa na Zanzibar yameanza.

“Haya yanayotukuta ni makubwa, tunachokiomba hawa watu wakamatwe mbona majambazi yanakamatwa, liwe fundisho, bila kufanya hivyo hili jambo litaendelea hata kama sio kwa familia hii lakini kwa wananchi wengine,” amesema huku akipeleka kilio hicho kwa viongozi wakuu wa nchi.

Mjomba wa marehemu ambaye hakutaka jina lake litajwe, amesema kinachowasikitisha zaidi watu hao kujitambulisha wametoka kwenye vikosi na simu ilipopigwa wakajibiwa yupo kwenye mikono salama halafu wakaokota maiti.

Akizungumza na Mwananchi kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Richard Mchomvu bila kufafanua zaidi amesema wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo na ukikamilika zitatolewa taarifa zaidi.

“Tukio hilo lipo uchunguzi bado unaendelea, tukikamilisha tutaeleza zaidi,” amesema Mchomvu.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit

Dar es Salaam — Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has declared an outbreak of Marburg virus, confirming a single case in the northwestern region of Kagera after a meeting with WHO director-general Tedros Adhanom Ghebreyesus.

The confirmation follows days of speculation about a possible outbreak in the region, after the WHO reported a number of deaths suspected to be linked to the highly infectious disease.

While Tanzania’s Ministry of Health declared last week that all suspected cases had tested negative for Marburg, the WHO called for additional testing at international reference laboratories.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”Amelia Clemence, public health researcher

Subsequent laboratory tests conducted at Kagera’s Kabaile Mobile Laboratory and confirmed in Dar es Salaam identified one positive case, while 25 other suspected cases tested negative, the president told a press conference in Dodoma, in the east of the country today (Monday).

“The epicentre has now shifted to Biharamulo district of Kagera,” she told the press conference, distinguishing this outbreak from the previous one centred in Bukoba district.

Tedros said the WHO would release US$3 million from its emergencies contingency fund to support efforts to contain the outbreak.

Health authorities stepped up surveillance and deployed emergency response teams after the WHO raised the alarm about nine suspected cases in the region, including eight deaths.

The suspected cases displayed symptoms consistent with Marburg infection, including headache, high fever, diarrhoea, and haemorrhagic complications, according to the WHO’s alert to member countries on 14 January. The organisation noted a case fatality rate of 89 per cent among the suspected cases.

“We appreciate the swift attention accorded by the WHO,” Hassan said.

She said her administration immediately investigated the WHO’s alert.

“The government took several measures, including the investigation of suspected individuals and the deployment of emergency response teams,” she added.

Cross-border transmission

The emergence of this case in a region that experienced Tanzania’s first-ever Marburg outbreak in March 2023 has raised concerns about cross-border transmission, particularly following Rwanda’s recent outbreak that infected 66 people and killed 15 before being declared over in December 2024.

The situation is particularly critical given Kagera’s position as a transport hub connecting four East African nations.

Amelia Clemence, a public health researcher working in the region, says constant vigilance is required.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”

The Kagera region’s ecosystem, home to fruit bats that serve as natural reservoirs for the Marburg virus, adds another layer of complexity to disease surveillance efforts.

The virus, closely related to Ebola, spreads through contact with bodily fluids and can cause severe haemorrhagic fever.

Transparency urged

Elizabeth Sanga, shadow minister of health for Tanzania’s ACT Wazalendo opposition party, says greater transparency would help guide public health measures.

“This could have helped to guide those who are traveling to the affected region to be more vigilant and prevent the risk of further spread,” she said.

WHO regional director for Africa Matshidiso Moeti says early notification of investigation outcomes is important.

“We stand ready to support the government in its efforts to investigate and ensure that measures are in place for an effective and rapid response,” she said, noting that existing national capacities built from previous health emergencies could be quickly mobilised.

The situation coincides with leadership changes in Tanzania’s Ministry of Health, with both the chief medical officer and permanent secretary being replaced.

This piece was produced by SciDev.Net’s Sub-Saharan Africa English desk.

Source: allafrica.com

Continue Reading