Wadau waonyesha kasoro ulaji mbogamboga, matunda

Dar es Salaam. Wakati ulaji wa mbogamboga na matunda ukitajwa kuwa moja ya njia ya kujenga mwili wa binadamu na kumuepusha na magonjwa, imeelezwa mboga nyingi zinazozalishwa hazifai kwa ajili ya matumizi ya binadamu.

Hiyo ni kutokana na kuwa na bakteria wanaoweza kuathiri matumbo ya watu na viuatilifu vilivyozidi kiwango.

Hayo yamesemwa leo Jumatatu, Julai 22, 2024 katika mjadala wa X Space ulioandaliwa na Mwananchi kwa kushirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) pamoja na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) wenye mada inayosema: ‘Mambo muhimu ya kuzingatia katika uandaaji, ulaji wa mbogamboga na matunda.’

Akizungumza katika mjadala huo, Mtaalamu wa Kituo cha Mbogamboga duniani, Jeremiah Sigalla amesema kupitia ukaguzi waliofanya waligundua baadhi ya mboga katika masoko ya Arusha na Dar es Salaam zilikuwa chafu na zinahatarisha afya ya mlaji.

Mtaalamu huyo amesema katika taasisi yao ya World Vegetable Centre kupitia tafiti walizozifanya wamegundua mboga hizo zina kiwango kikubwa cha wadudu wanaodhuru tumbo.

“Kupitia kuangalia viambata ambavyo vinaathiri lishe na afya ya mlaji, mboga hizi zimekuwa na kiwango kikubwa cha bakteria wanaodhuru mazingira ya tumbo na katika baadhi ya masoko ya Arusha ya Dar es Salaam tumekuta mboga nyingi ambazo zinaonekana nzuri kwa macho ukazinunua, lakini kwa afya si salama,” amesema Jeremiah.

Amesema kwa kuwa maeneo mengi ya mijini mboga hizo zinahitajika kwa wingi, ndio maana hata mazingira ya uzalishaji wake si salama.

Hivyo amesema kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kama FAO wanaona ni muhimu elimu kutolewa kwa wakulima katika matumizi ya dawa ambazo zinatumika kuzitunza mboga hizo.

“Kuna baadhi ya dawa na mbolea maarufu kama busta zinachangia uharabifu wa hizi mboga. Teknolojia inakua, lakini njia za teknolojia hiyo kama mzalishaji asipopata taarifa sahihi itaathiri uzalishaji na tija inayopatikana katika uzalishaji wake,” amebainisha Sigalla.

Katika hilo, Mtafiti na mtaalamu wa chakula, Martin Kimanya amesema mtu anapokula mbogamboga zilizochafuliwa ikiwemo kemikali ni sawa na kutokuwa navyo nyumbani.

“Tatizo kubwa lililopo nchini katika eneo la mbogamboga ni uchafuzi kutokana na matumizi ya viuatilifu katika kiwango ambacho si bora,” amesema.

Amesema kuwa pia kuna wakulima wanataka kuongeza uzalishaji, lakini wamekuwa wakifanya katika namna ambayo haifai na wengi hawana ufahamu ambao utawafanya wajue ni aina gani ya viuatilifu si sahihi vya kutumia.

“Kwa bahati mbaya udhibiti wa viatilifu vilivyopo sokoni kwetu pia si mzuri, kwani baadhi vinaweza kuwa vimepigwa marufuku huko nje, lakini bado vikawepo sokoni huku wakulima wakikosa mbinu sahihi ya kutumia viatifu hivyo,” amesema Profesa Kimanya.

Amesema ukubwa wa hili tatizo unatokana na mambo matatu la kwanza ni wakulima kutumia viatifu ambavyo baadhi haviruhusiwi na hawajui namna nzuri ya kuvitumia, maofisa ugani na kilimo kutokuwa na uwezo wa kumfikia mtu kwa namna inayotakiwa ili kumueleza namna nzuri ya utumiaji ili kutoathiri afya ya mlaji.

Alichokisema Malembo

Kuhusu maofisa ugani kuhudumia wakulima, Mkurugenzi wa Malembo Farm, Lucas Malembo amesema utafiti uliofanywa na Jukwaa Huru la Kilimo ANSAF mwaka 2017 umeonyesha asilimia 48 ya vijiji 15,082 vilivyosajiliwa nchini havina maofisa ugani wa kutosha.

Utafiti unaonyesha pengo hilo wakati ambao sera ya kilimo ya mwaka 2013 ikitaka kila kijiji kuwa na afisa ugani mmoja.

“Katika hali ya kawaida bado kuna changamoto ya usalama wa mboga tunazokula kutokana na uhaba wa watalaamu. Matumizi mabaya ya viuatilifu ni matokeo ya wakulima wengi kutokuwa na elimu ya kilimo biashara sensa ya kilimo ya mwaka 2019/2020 inaonyesha matumizi ya viuatilifu ni asilimia mbili ya wakulima wote nchini,” amesema.

Hata hivyo, Profesa Kimanya amesema kutokana na kutokuwa na uhakika na usalama wa tunda linapotoka ni vyema kuliosha na kulimenya kabla ya kuanza kula.

Kuosha na kumenya kunapunguza kemikali ambazo zinapatikana, ijapokuwa utapunguza baadhi ya virutubisho katika tunda hilo.

Faida za tunda

Pamoja na changamoto hizo, Mkurugenzi Idara ya Elimu na Mafunzo ya Lishe kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC,) Dk Esther Nkuba amesema mwili wa binadamu unahitaji virutubisho zaidi ya 50 kwa siku na kila chakula kina virutubisho zaidi ya kimoja, hivyo ulaji wa matunda wakati wa kula iwe asubuhi mchana au jioni hauna tatizo.

“Hakuna tafiti inayosema ukila matunda kwa kuchanganya inatengeneza sumu. Ukila ndizi ukachanganya na parachichi mwili wenyewe unajua chakufanya,” amesema Dk Nkuba.

Akichangia hoja hiyo, Mkurugenzi wa Hospitali ya Muhimbili, Profesa Mohammed Janabi amependekeza watu kupenda kula matunda yenyewe badala ya kunywa juisi, ili kupunguza wingi wa sukari anayoweza kuinywa kwa wakati mmoja.

“Pia watu wale vyakula badala ya kutumia dawa za virutubishi, kwani haviwezi kuwa mbadala wake,” amesema Profesa Janabi.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Zanziba, Dk Omar Ally Amir amesema katika kukabiliana na changamoto hizo wanachokifanya sasa ni kuangalia namna wanayoweza kuwafikia wakulima, ili kuzalisha mbogamboga na matunda ambayo ni salama kwa walaji.

“Pia tunajaribu kuhimiza kilimo hai kisichotumia viuatilifu, ili mazao yanapozalishwa yawe salama kwa watumiaji,” amesema Dk Amir.Continue Reading

Tanzania’s President Samia Suluhu fires foreign, information ministers

By REUTERS

Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has fired two senior members of government including the foreign minister in a mini-cabinet reshuffle, her office said.

The changes came as Hassan seeks to regain trust from foreign powers over a programme of economic and political reforms, including easing restrictions on opposition parties and media, that some critics had seen as faltering.

The presidency announced late on Sunday, July 21, that Hassan terminated the appointments of the minister of foreign affairs and East Africa cooperation, January Makamba, and the minister of information, communication and information technology, Nape Nnauye.

They are influential figures in the ruling party, Chama cha Mapinduzi (CCM).

No reason was given for their removal. Makamba and Nnauye did not immediately respond to requests for comment.

Read: Samia replaces TRA chief amid diplomats, traders tax complaints

Advertisement

The dismissal of Nnauye comes a week after comments he made surfaced in a video, saying elections results would depend on who counts votes and announces the results.

Nnauye later apologised, saying it was a joke, but activists and some social media users said the statement undermined Hassan’s push to improve democracy.

Also read: Will sacked minister Nnauye join rebellion in CCM?

Hassan appointed Mahmoud Thabit Kombo as new foreign affairs minister and Jerry Silaa as minister of information, communication and information technology.

Before Kombo’s appointment, he was Tanzania’s ambassador to Italy while Silaa was the minister of lands, housing and human settlements development. Two more ministers and deputy ministers were also appointed, the presidency said.

In power since 2021, Hassan’s government has won praise for rolling back her predecessor’s crackdowns on the opposition and civil rights groups. But arrests last year of a lawyer and an opposition politician have raised questions over her government’s human rights record.

Continue Reading

Rais Samia asimulia machungu mpunga wake ulivyoliwa na mifugo

Dodoma. Rais Samia Suluhu Hassan ameelezea machungu wanayokutana wakulima kwa mazao yao kuliwa na mifugo, huku akasimulia majibu ya dharau aliyopewa na mfugaji baada ya mifugo kula mpunga katika shamba lake, eneo la Dutumi, Mkoa wa Morogoro.

Akizungumza leo Julai 20, 2024 wakati akizungumza na machifu nchini, Rais Samia amesema kuna migogoro kati ya wakulima na wafugaji ambapo watu wamekuwa wakipigwa, kuuana na mazao yao kuliwa na mifugo.

“Niwaombe sana machifu wenzangu tukayasimamie haya. Tunapoacha wakulima na wafugaji wakauana na mara nyingi wanaoonewa ni wakulima, hii si haki. Nitakupeni mfano ulionipata mimi mwenyewe,” amesema.

Amesema aliwahi kulima mpunga katika eneo la Dutumi, Mkoa wa Morogoro na kwamba alilima mara ya kwanza kwa kuweka fedha yake yote kwenye shamba hilo.

“Basi wakaja watu na ng’ombe wao, mpunga umenawiri, nishasema hapa umasikini bye bye (kwa heri), dakika 10 nyingi mpunga wote ukaingia ng’ombe kama 300, wakaula. Sikuweza kufanya kitu chochote,” amesema.

Hata hivyo, amesema watoto wake walimweleza kuwa wajaribu tena kulima kwenye shamba hilo na hivyo akaamua kulima nusu ya eneo alilolima awali.

Amesema lakini mpunga ulivyoanza kuchanua na kuvutia na ukaanza kutoa harufu, ng’ombe waliingia tena katika shamba na kuula tena.

“Tulipokwenda katika kesi, mara hii nikasema hapana. Nikachukua mtendaji wa kijiji, polisi, sijui nani nikasema twende. Tulipokwenda katika kesi mfugaji anasema ng’ombe wangu kala mpunga wapi? Aliingia katika ghala ya nani, amekula majani tu,” amesema.

Rais Samia amesema inapotokea dharau ya namna hiyo ambayo inatolewa kwa mtu ambaye ameshapoteza nguvu na fedha na jasho, haileti amani Tanzania.

“Mfugaji anasema ng’ombe amekula majani tu, hajaingia katika ghala kula mpunga wa mtu. Sasa mambo kama haya yakitokea hayaleti amani Tanzania. Niwaombe sana machifu katika maeneo yetu tukayasimamie hayo,”amesema.

Aidha, Rais Samia amewataka Watanzania, viongozi wa Serikali, taasisi zisizo za kiserikali, viongozi wa kidini na machifu, kukemea vitendo viovu vinavyokiuka maadili ya Kitanzania.

“Tunapoona vitendo vya ovyo katika maeneo yetu, machifu tusemeni, tukemee. Kama mnamuona mkuu wenu wa wilaya hafanyi vyema mkemeeni, msemeni, muumbueni tumjue. Kama mnamuona kiongozi haendi mwendo mwema tuambieni tumjue ili tulete viongozi waadilifu na mambo yaende vizuri,” amesema.

Amesema mwongozo kwa ajili ya kuratibu shughuli za machifu nchini unaandaliwa, ambao ndio utaweka utaratibu wa kuwasema viongozi wanaokiuka maadili na sio kusimama na kuropoka.

“Niwaombe twende tukakemee vitendo viovu vinavyokiuka maadili yetu. Tudumishe upendo, amani, utu na kuheshimiana,” amesema.

Pia amewataka Watanzania wanapohama kutoka eneo moja kwenda jingine, kufuata mwongozo unaowataka kuchukua barua wanapotoka na kupeleka wanakokwenda ili kuwatambulisha.

“Lakini watu wanahamishana usiku na malori, wao na wanyama, wakifika mahali wanateremshana, pengine kuna mwenyeji anawasubiri wanavamia mapori, wanavamia misitu wanaingia huko,wengine wanafyeka mapori,” amesema.

Naye, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro amesema kwa sasa Serikali iko katika hatua za mwisho ya kuandaa mwongozo wa kutambua machifu na viongozi wa kimila, ili waweze kupata heshima wanayostahili kwa jamii na Serikali kwa ujumla.

“Mwongozo unaoandaliwa utatambua machifu na viongozi wa kimila katika ngazi ya wilaya na mikoa ili kutoa fursa kwa machifu kutekeleza jukumu lao la msingi la kuwawezesha Watanzania kuendelea kupata haki yao ya kikatiba na uhuru wa kuabudu kupitia mila, desturi na imani za kijadi,” amesema.

Aidha, Dk Ndumbaro amesema taarifa za uchumi za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), mwaka 2023 zinaonyesha kuwa sekta ya utamaduni na sanaa inaongoza kwa kukua nchini ambapo imekuwa kwa asilimia 17.7.

Awali, Mwenyekiti wa Umoja wa machifu wa Tanzania, (UMT), Antonia Shangalai amesema kuwa Rais Samia amepandisha hadhi ya wanawake wa Tanzania kwa kuwapandisha vya kutosha na kuwataka mawaziri kutoa ushirikiano wa kutosha kwake.

“Sisi machifu tuko nyuma yenu tutaenzi mila, kuheshimiana, kuwaheshimu wakubwa na mambo yote yanayokwenda na mila na desturi zetu tusiyoyataka na nyie hamyataki na Serikali haiyataki. Tunaendelea kupambania hayo yasiendelee kuwepo kabisa,”amesema.

Akitoa baraka za machifu, Chifu Rocket Mwashinga amesema wakati nchi inaelekea kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu, anahimiza Watanzania kulinda amani ya nchi na kuonya suala la ukabila.Continue Reading