TFA secures $150m to boost Tanzania’s agricultural sector
The factory is expected to significantly enhance domestic production of cooking oil.Continue Reading
The factory is expected to significantly enhance domestic production of cooking oil.Continue Reading
The initiative forms part of the bank’s broader ambition to plant 6,000 trees across the country by the end of this year.Continue Reading
Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema nafasi ya aliyekuwa Mkurugenzi mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Dk Faustine Ndugulile itaelekezwa kwa Mtanzania mwingine mwenye sifa.
Rais Samia amesema hayo leo Jumatatu Desemba 2, 2024 katika hafla ya kuaga mwili wa Dk Ndugulile, aliyekuwa mbunge wa Kigamboni iliyofanyika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam.
Dk Ndugulile alifariki dunia Novemba 27, 2024 nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu. Mwili wake utazikwa kesho Jumanne, katika makaburi ya Mwongozo, Kigamboni.
Alifikwa na mauti ikiwa imesalia miezi michache kwenda kuanza kutumikia nafasi yake mpya WHO Februari, 2025. Alichaguliwa kwenye nafasi hiyo Agosti 2024, akiweka rekodi ya kuwa Mtanzania na mwana Jumuiya ya Afrika Mashariki wa kwanza.
Katika salamu zake, Rais Samia amesema nchi ilimpata mwakilishi: “Wanadamu tunapanga yetu, lakini Mungu anatupangia, Dk Ndugulile ameiweka nchi pazuri lakini Mungu amechukua kilicho chake.
“Tutaingia tena kwenye mashindano tutatafuta Mtanzania mwenye sifa anayeweza kushindana na ulimwengu, tutaingia tena na tutaweka mtu mwenye sifa ileile kutuwakilisha,” amesema Rais Samia.
Rais Samia amesema amepokea salamu nyingi za pole kutoka ndani na nje ya nchi, huku akiwashukuru viongozi waliofika kumuaga Dk Ndugulile hasa kutoka WHO.
“Mengi yamesemwa na tumeyasikia mengi katika mchango wake kwa nchi na duniani, uongozi wake, mchango wake katika taaluma ya tiba na siasa hasa kwa wananchi wa Kigamboni,” amesema.
Rais Samia amesema wajibu wa nchi ni kuimarisha uwakilishi wa Tanzania ndani ya nchi na Afrika hasa katika Shirika la Afya Duniani.
“Katika kuimarisha ushiriki wetu ni azma ya Serikali kuhakikisha sasa Watanzania wabobezi tunaweka kila aina ya nguvu watuwakilishe katika fani za kimataifa.
“Dk Ndugulile alikuwa mwanamajumuia kutokana na imani yake ndicho kilichomsukuma akagombee nafasi hiyo na Serikali ikamuunga mkono tukajaliwa kupata nafasi ile, mwanadamu hupati unachokipata unapata majaliwa,” amesema Samia.
Walichokisema WHO
Awali, Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani WHO Kanda ya Afrika, Dk Matshidiso Moeti amesema Dk Ndugulile alikuwa na maono ya kufanya mageuzi makubwa katika shirika hilo.
Amesema tangu aliposhinda nafasi yake Agosti 2024, alishaanza kuandaa namna atakavyoliongoza Bara la Afrika katika nafasi yake mpya.
Amesema kupitia nafasi yake, tayari alianza kuandaa mambo kadhaa kwa kushirikiana na ofisi yake.
“Alitutembelea mwezi uliopita na alizungumza nasi mambo mengi kuhusu kile atakachokuja kukifanya na mageuzi anayoyataka. Tulijiandaa kufanya vizuri zaidi katika uongozi wake na wengi walijiandaa wakiwemo wafanyakazi na wengine ambao tumekuwa tukifanya nao kazi,” amesema Dk Moeti.
Kwa mujibu wa Dk Moeti, taarifa za kifo cha Dk Ndugulile ziliwashtua si tu ofisi ya WHO Afrika iliyopo Brazzaville DRC Congo, bali katika ofisi kuu za WHO Geneva, Uswisi.
“Leo nimeongozana na viongozi wengi, wakiwemo wakurugenzi wa WHO Afrika, mawaziri wa afya na washirika wengine.
“Baada ya taarifa za kifo, nilipokea meseji nyingi na simu kutoka nchi mbalimbali duniani. Machozi ni ya wengi kuondoka kwa Dk Ndugulile na wengi wameumia kuona kiongozi mwenye maono anaondoka bila kutumikia nafasi yake,” amesema Dk Moeti.
Amesema wakati huu wa majonzi ni kubaki kushangilia maisha yake, kwani ni mtu aliyekuwa na uwezo mkubwa katika afya ya umma na waliamini uwezo wake angeutumia zaidi katika sera za kiafya kuhakikisha analeta mabadiliko Afrika.
Dk Moeti amesema kifo cha Dk Ndugulile kimemtonesha kidonda cha Dk Mwele Malecela.
“Kwa niaba ya WHO natoka pole kwa Tanzania na Serikali ya Tanzania na Rais wa Jamhuri ya Jamhuri ya Tanzania, watoto na mke wake,” amesema Dk Moeti.
Tamsa, MAT wamlilia
Chama cha Madaktari Wanafunzi Tanzania na (Tamsa) na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) wamesema wataenzi mema aliyoyaacha Dk Ndugulile.
Akisoma salamu za Tamsa, Makamu wa rais wa chama hicho, Dua Almas amesema walizipokea taarifa za kifo cha cha mlezi wao Dk Ndugulile kwa masononekana na wanahisi wamepoteza kioo kuelekea kutimiza ndoto zao.
“Dk Ndugulile alikuwa mwanachama hai na alihudumu nafasi mbalimbali katika chama chetu, ikiwemo katibu mkuu na alipohitimu masomo aliendelea kuwa mwanachama na kutoa michango yake, alikuwa anatupa moyo siku moja tunaweza kufanikiwa zaidi yake,” amesema Almas.
Amesema Dk Ndugulile alikubali kuwa mlezi wa chama hicho tangu 2023 na alikuwa msaada mkubwa, hivo kifo chake ni pigo kwao.
Kwa upande wake, rais mteule wa MAT, Dk Alex Msyoka amesema Dk Ndugulile alikuwa daktari bingwa wa afya ya jamii pamoja na kwamba alikuwa mwanasiasa, hakuweka kando taaluma yake.
“Tutamkumbuka kwa mambo mengi, ikiwemo alipokuwa mstari wa mbele kukabiliana na ugonjwa wa Uviko 19, na alikuwa kinara kwenye kupambana ya maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi,” amesema Dk Msyoka.Continue Reading
Speaking at an event to mark the 20th anniversary of beverage company Mega Beverages over the weekend, Mr Teri said the firm has set an example that Tanzanian companies are capable of succeedingContinue Reading
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Taifa cha Uwekezaji (TIC) Gilead Teri amesema huenda mwaka huu Tanzania ikavunja rekodi ya kujasili miradi mingi ya uwekezaji iliyodumu kwa miaka 11.Continue Reading
Dar es Salaam. Wakati Tanzania ikiungana na mataifa mengine duniani katika kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, moja ya vitu vinavyotajwa kuchochea ukatili huo ni ndoa za utotoni.
Miongoni mwa changamoto zinazotokana na ndoa za utotoni ni unyanyasaji wa kimwili, ikizingatiwa wanaoolewa kuna nyakati hukumbana na vipigo na mateso kutoka kwa wenza wao na hata ndugu, hivyo kukiuka haki zao za msingi.
Si hayo pekee, ndoa hizi husababisha ukatili wa kijinsia wa kihisia na kisaikolojia. Watoto wanaolazimishwa kuingia kwenye ndoa mara nyingi wanakosa uwezo wa kujieleza, kushiriki maamuzi ya familia, au kudai haki zao. Wanapozuiliwa kujieleza, wanapewa jukumu la kuwatunza watoto au familia wakiwa bado hawajakomaa, jambo linalowaathiri kisaikolojia.
Pia husababisha unyanyasaji wa kiuchumi, watoto hukosa fursa ya kupata elimu na kushiriki katika shughuli za kiuchumi.
Kukosa elimu na fursa za kiuchumi kunawaweka katika hali ya utegemezi wa kifedha kwa waume zao, hivyo kusababisha hatari ya kunyanyaswa kijinsia kwa kutokuwa na uwezo wa kujitegemea.
Ni kutokana na ndoa hizi, watoto huathiriwa kwa kuzaa mapema kabla miili yao haijakomaa, hali ambayo huongeza hatari ya matatizo ya kiafya kama vile fistula, kifafa cha mimba na hata vifo vya uzazi.
Ndoa za utotoni huwanyima wasichana nafasi ya kujenga mahusiano yenye usawa, badala yake, wanajikuta wakitumikishwa nyumbani, na kubaguliwa.
Kwa mujibu wa Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya
Malaria Tanzania (TDHS-MIS) mwaka 2022, asilimia 20.3 ya Watanzania wenye miaka 15-19 wameolewa, wanaishi pamoja au walikwisha kuwa kwenye mahusiano na wametengana. Kati ya walioolewa wa umri huo asilimia 30.6 wanandoa zilizosajiliwa na wana vyeti.
Vilevile takwimu hizo zinaonyesha wanawake wenye miaka 25-49 waliolewa wakiwa na wastani wa miaka 19.8.
Utafiti unaeleza elimu na hali ya umasikini vinachangia kwa kiwango kikubwa, kwani wastani wa umri wa wanawake wasio na elimu na ni masikini kuolewa ni miaka 18.1 ukilinganisha na wale waliohitimu sekondari au elimu ya juu walioolewa na miaka 23.7.
Hata hivyo, takwimu zinaonyesha wanawake huanza kujihusisha na ngono miaka mitatu kabla ya kuolewa wakiwa na wastani wa miaka 17 na wanaolewa wakiwa na miaka 19.8.
Baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa na maoni mbalimbali yanayopingana na ndoa za utotoni.
Padri Longino Rutangwelera anasema Kanisa Katoliki haliungi mkono ndoa hizo, akieleza maana ya ndoa katika mustakabali wa dini.
Padri Rutangwelera anasema katika dini ndoa ni maagano ya watu wawili waliokomaa kimwili na kiakili na si vinginevyo.
“Ndoa ina wajibu wake, misingi na haki zake inamtaka mtu awe na ukomavu wa kiakili na kiimani pia, unapomlazimisha msichana kuingia kwenye ndoa za utotoni unapingana na uhalisia,” anasema.
“Kumuoza binti ambaye hajakomaa kiakili, kimwili na kifikra ni kupingana na matakwa na mapenzi ya Mungu na kupingana na uhalisia.
“Unapomlazimisha mtoto kuingia katika ndoa anakosa elimu na kuingizwa kwenye makubaliano ambayo kwa akili na ukomavu wake hana uelewa wa kutosha, hivyo atapata watoto wakati uwezo wake wa kuwa mama au baba hautoshi, ni vema wakaachwa hadi wawe wakomavu, kimwili, kiakili na kihisia ili kupokea majukumu hayo kikamilifu,” anasema.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), Sheikh Khamis Mataka anasema kuna umuhimu wa kutenda uadilifu kwa kuwapa nafasi sawa watoto wa kiume na wa kike, ikiwamo suala zima la kupata elimu kwa kadri ya uwezo wao.
“Hata hivyo, bado kuna changamoto kwa mtoto wa kike, ikiwamo ya kuozwa katika umri mdogo na kukosa haki yake ya kielimu.
“Ninachokitamani ili kuondoa ukatili huu, kuwepo sheria ambayo itamsaidia mtoto wa kike kutoingia kwenye ndoa za utotoni,” anasema.
Akifafanua kuhusu Sera ya Elimu ya mwaka 2014, Sheikh Mataka anasema imeweka kidato cha nne kuwa ni elimu ya lazima.
Kiongozi huyo anasema kama sera itaongezwa na kudadavua kwamba elimu ya lazima iwe kidato cha sita, itamsadia mtoto wa kike.
“Hadi atakapohitimu kidato cha sita, huyu mtoto atakuwa amefikisha miaka 17 hadi 18, katika umri huu changamoto cha ndoa za utotoni itakuwa imeondoka,” anasema.
Anasema Sheria ya Ndoa namba 5 ya mwaka 1971 nayo itamke mwanafunzi wa elimu ya lazima haruhusiwi kuoa wala kuolewa na Sheria ya Elimu namba 5 ya mwaka 1978 iseme mtoto haruhusiwi kuoa wala kuolewa hadi ahitimu elimu ya lazima, hivyo itasaidia kuwalinda watoto wa kike.
“Atakapohitimu elimu ya lazima atakuwa amepata ukomavu ambao hata akiolewa atakuwa na uwezo wa kulea familia,” anasema.
Mchugaji Monica Lugome wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani anasema ajenda kubwa ya kumlinda mtoto wa kike na ndoa za utotoni ni kutoruhusu aolewe chini ya miaka 18.
Anasema anapoolewa chini ya umri huo ni mateso kwake na hata vitabu vya dini haviruhusu hilo.
“Biblia inatuagiza kumlea mtoto katika njia impasayo ikiwamo kuhakikisha anapata haki zake katika nyanja zote ikiwamo elimu. Unapomuoza katika umri mdogo ni kumnyima haki yake ya msingi,” anasema Mchungaji Monica.
Mjadala wa kitaifa
Taasisi ya kimataifa ya Norwegian Church Aid iliandaa mjadala wa kitaifa kujadili umri sahihi wa kuoa au kuolewa, uliowahusisha wadau mbalimbali kutoka mikoa 10 nchini.
Msimamizi wa miradi wa taasisi hiyo Tanzania, Sarah Shija anasema mjadala huo uliofanyika Novemba 28, ulilenga kukosoa na kushauri kuhusu changamoto zinazosababisha ukatili wa kijinsia.
“Hii itasaidia kuleta mabadiliko, kuna makundi kama viongozi wa dini yana nafasi na ushawishi katika mabadiliko ya kisheria, hususani kwenye umri wa binti kuolewa na madhara ya ndoa katika umri mdogo,” anasema.
Rebeca Gyumi, Mkurugenzi wa Taasisi ya Msichana Initiative anasema pamoja na mambo mengine, mjadala huo pia umeangalia uzoefu wa nchi mbalimbali kwenye masuala ya mabadiliko ya umri wa ndoa.
Rebeca aliyefungua kesi za kikatiba kupinga vifungu vya 13 na 17 vya Sheria ya Ndoa vilivyotoa mwanya kwa watoto wa kike kuolewa wakiwa na umri wa miaka 14 kwa kibali cha Mahakama na umri wa miaka 15 kwa ridhaa ya wazazi, anasema mchango wa viongozi wa dini ni mkubwa ili kufikia lengo la kutokomeza ukatili wa kijinsia, hususani ndoa za utotoni.
Rachel Boma, kutoka Shirika la UN Woman Tanzania anasema nchi mbalimbali zimefanya mabadiliko ya kisheria na kuweka umri wa ndoa kuwa miaka 18.
“Nchi kama Indonesia au Misri ambazo mfumo wao wa sheria ni kama kwetu, Serikali ziliona mabadiliko katika sheria zao na wao umri wa kuolewa ni miaka 18, hivyo katika mijadala kama hii tuna vitu vingi vya kujifunza kutoka kwa wenzetu.
Akizindua kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi, alisema Serikali itayajadili maombi yote yaliyotolewa na mtandao wa kupinga ukatili wa kijinsia (Mkuki) ikiwamo suala la kutunga sheria mahususi ili kushughulikia masuala ya ukatili wa kijinsia na kuyatokomeza.
Alisema watakaa pamoja kuyajadili ili kuona namna gani hatua mbalimbali zinaweza kuchukuliwa.
”Katika sheria zetu mbalimbali tuna sheria nyingi zinazopinga ukatili wa kijinsia na zinaelezea masuala hayo na kutoa adhabu kali ikiwemo Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 mkiisoma sheria hiyo imeelezea ukatili katika maeneo mengi,” alisema.
Kampeni hiyo iliyozinduliwa Novemba 23 itafikia tamati Desemba 10. Kaulimbiu ni ‘Kuelekea miaka 30+ ya Beijing, Chagua kutokomeza ukatili.’
Kaulimbiu hiyo inawakumbusha watu kujitafakari na kitathmini yale yanayofanywa kama yana tija.
Mwenyekiti wa Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WiLDAF), Dk Monica Muhoja anasema kuna haja ya kutungwa sheria maalumu kupinga ukatili wa kijinsia.
“Mwaka huu tumekuja na maombi mengine ikiwamo kufika kwenye ajenda za kiusalama kuhakikisha masuala ya ukatili wa kijinsia yanaingizwa rasmi katika mipango na mikakati ya kiusalama ya kitaifa,” alisema.
Mkurugenzi wa WiLDAF, Anna Kulaya alisema dhamira ya kampeni hiyo ni kushawishi na kuhamasisha jamii kuondoa mitazamo inayochochea unyanyasaji na ukandamizaji wa kijinsia huku ikikuza usawa, heshima na haki kwa wote.Continue Reading
The Zanzibar government has reaffirmed its commitment to supporting the USAID Kizazi Hodari Southern Zone Project, which focuses on improving the health, well-being, and protection of orphans and vulnerable childrenContinue Reading
The loan is equivalent to Sh198.75 billion disbursed for the project scheduled to be implemented over five years (2025-2029).Continue Reading
A survey by the East African Business Council, the private sector arm of the East African Community, indicates that the overall ease of doing business in the region deteriorated with all eight indicators declining compared to 2023.
In details contained in the 2024 Ease of Doing Business in the East African Community (EAC) survey, the East African Business Council (EABC) noted that the ease of doing business in the region was rated moderate, with an average rank of 3.22, which was a decline of 0.13 points compared to the 2023 rank of 3.09.
The ease is measured on a scale of one to five, of which, one represents very easy, while five represents very hard.
“The survey revealed that the overall ease of doing business within the EAC was moderate. The enterprises’ perception of the ease of doing business in 2024 shows a decline in all eight indicators in comparison to 2023,” the survey, which targeted companies involved in trade in goods and services across the region, and received a total of 300 responses, of which 201 were valid for analysis, reads in part.
Out of the 201 responses, 113 were from companies engaged in trade in goods, representing 56 percent, while 88 or 44 percent were from businesses involved in trade in services.
All eight indicators registered a decline in comparison to 2023, with government operations declining by 0.19 to 3.60, while removal of trade restrictions declined by 0.18 to 3.55.
Regulations for starting and operating a business in the region declined by 0.17 to 2.83, trade finance by 0.14 to 3.60, trading across borders by 0.14 to 3.26, and making cross-border payments by 0.14 to 2.87.
Infrastructure development declined by 0.04 to 2.80, while ease of paying taxes declined by 0.02 to 3.23.
The individual score for the eight surveyed indicators is key in determining the average score for the ease of doing business across the eight East African member states, among which include Uganda, Kenya, Tanzania, Rwanda, Burundi, DR Congo, South Sudan, and Somalia.
The survey indicates that Kenya and Tanzania registered the highest number of respondents – each 50 companies – while Uganda and Burundi registered responses from 34 and 23 companies, respectively.
Rwanda registered responses from 19 companies, DR Congo (13 companies), and South Sudan (eight companies).
In terms of country ranking, Rwanda scored better than other East African partner states, posting a score of 2.83 – which is perceived as easy – followed by Burundi, whose 3.02 score makes it a moderately easy country in doing business.
Kenya scored 3.19, Uganda (3.27), South Sudan (3.28), DR Congo (3.39), and Tanzania (3.39), all of which were ranked as moderate.
The decline was mainly due to deteriorations in several sub-indicators, including access to information on business fees, levies, and charges for startups, affordability of interest rates, implementation of the EAC Common External Tariff, ease of receiving payments from government, securing government tenders and import and export procedures, among others.
Interviewed businesses indicated that making cross-border payments and regulations for starting and operating businesses were moderate, while it was hard to remove trade restrictions, and obtain trade finance, and government operations.
However, ease of paying taxes, in particular compliance with tax requirements, improved from moderate (3.08) to easy (2.82), while infrastructure development, in particular access to affordable voice and data calls, slightly improved from 2.61 in 2023 to 2.57.
Other improvements were registered in recognition of professional qualification across the region and the availability of foreign currencies, in particular US dollars.
The improvements, the survey noted, were driven by the automation of tax payment systems making it easier for businesses across the region to comply with tax requirements, the EAC One Network Area, and monetary measures taken by governments across the region to increase the supply of US dollars.
Positive progress
Companies across East Africa also reported positive progress in the business environment, characterised by continuous government reforms and commitment to enact business-friendly laws, favourable political and economic stability, enhanced government collaboration with the private sector in policy formulation and investments through public-private partnerships, increased investment in infrastructure, human capital and active participation in regional and continental integration.Continue Reading
Dar es Salaam. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ataongoza matembezi ya hisani kwa ajili ya kuelimisha jamii kuhusu watu wenye ualbino.
Matembezi hayo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Lions Club ya Dar es Salaam, Tanzanite na Sky kwa kushirikiana na Chama cha wenye ualbino Tanzania (TAS), yatakwenda sanjari na uchangiaji wa fedha kwa ajili ya kusaidia mahitaji ya kibinadamu kwa kundi hilo.
Akizungumzia matembezi hayo yaliyopewa jina la Sunset Charity Walk, Kaimu Mwenyekiti wa TAS, Abdillah Omar amesema watu 1,000 wanatarajiwa kushiriki kwenye matembezi hayo.
Matembezi hayo ya kilomita tano yatafanyika kesho, Jumamosi ya Novemba 30, 2024 saa 11 jioni, kuanzia Ocean Road kwenda hadi daraja la Tanzanite.
“Tunaamini watu wengi watajitokeza kuungana nasi kutuunga mkono katika matembezi haya ambayo tunayafanya kwa mara ya kwanza kwa kushirikiana na Lions Club,” amesema.
Gavana wa Lions Club Tanzania, Habil Khanbhai amesema hii itakuwa mara ya kwanza kwa taasisi hiyo kusaidia watu wenye ualbino na wanatarajia kuendelea kushirikiana nao na kuwaunga mkono.
Mbali na elimu itakayotolewa kwa jamii ili ipate uelewa kuhusu watu wenye ualbino, pia matembezi hayo yanalenga kukusanya fedha kwa ajili ya kusaidia mahitaji mbalimbali ya kibinadamu kwa kundi hilo.
“Tunatarajia kuwa na watu 300 wenye ualbino, watu 100 kutoka Jeshi la Polisi na watu wengine kutoka maeneo mbalimbali,” amesema Khanbhai akisisitiza jamii kujitokeza kwa wingi kushiriki na kuliunga mkono kundi hilo sambamba na kujisajili kwa gharama ya Sh20,000.
Mkuu wa Utafiti wa Jeshi la Polisi, SACP Ralph Meela amesema jeshi hilo limekuwa likishirikiana kwa karibu na kundi hilo ikiwamo kuzielimisha jamii ambazo zimekuwa na imani potofu kuhusu ualbino.
“Kwa muda mrefu tumekuwa tukifanya hivi na hata matukio ya kikatili dhidi ya ndugu zetu hawa (wenye ualbino) yalitulia na tangu 2022 tulikuwa tumeyasahau, hivi karibuni ni kama yameibuka , tunaendelea kuyatokomeza,” amesema.Continue Reading
Zanzibar Investment News Tanzania Investors Ltd © 2025