Aliyeingia Tanzania bila kibali, atozwa faini ya Sh1 milioni

Aliyeingia Tanzania bila kibali, atozwa faini ya Sh1 milioni

Aliyeingia Tanzania bila kibali, atozwa faini ya Sh1 milioni

Dar es Salaam. Raia wa India, Devanshu Dusad (24) amehukumiwa kulipa faini ya Sh1 milioni au kutumikia kifungo cha miaka miwili jela, baada ya kupatikana na makosa mawili ikiwamo kuishi nchini Tanzania bila kibali.

Dusad amehukumiwa kifungo hicho, leo Jumanne Novemba 19, 2024, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya kukiri mashtaka yake mawili na Mahakama kumtia hatiani.

Hata hivyo, mshtakiwa huyo amefanikiwa kulipa faini hiyo na kukwepa kifungo.

Kabla ya kupewa adhabu hiyo, mshtakiwa huyo, alijitetea kuwa anaomba apunguziwe adhabu kwa sababu viza yake iliisha Oktoba na alikuwa katika utaratibu wa kutengeneza nyingine.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mkuu, Aaron Lyamuya, amesema mshtakiwa ametiwa hatiani kama alivyoshtakiwa.

“Kutokana na mshtakiwa kukiri shtaka lake mwenyewe bila kulazimishwa, Mahakama imezingatia upande wa mashtaka hawana kumbukumbu za makosa ya nyuma dhidi ya mshtakiwa, hivyo ina kuhukumu kulipa faini ya Sh 500,000 kwa kila shtaka au kwenda gerezani miezi 12 kwa kila kosa,” amesema Hakimu.

Awali, wakili kutoka Idara ya Uhamiaji, Ezekiel Kibona aliiomba Mahakama itoe adhabu kwa mujibu wa sheria ili iwe funzo kwa raia wa kigeni kuishi nchini bila kufuata utaratibu.

Akimsomea hati ya mashtaka, Wakili Kibona alidai kuwa, mshtakiwa huyo anadaiwa kutenda kosa hilo Novemba 13, 2024 katika ofisi za Commododities Tanzania Ltd zilizopo Mtaa wa Samora, jijini hapa.

Alidai siku hiyo ya tukio, mshtakiwa akiwa raia wa India alikutwa akiishi nchini bila kuwa na nyaraka yoyote inayoonesha  ni raia wa India huku akijua kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria. 

Shtaka la pili, siku na eneo hilo akiwa raia wa India, alikutwa akifanya biashara, bila kuwa na kibali cha kazi.

Mshtakiwa baada ya kusomewa shtaka na hoja za awali (PH)alikiri kutenda kosa hilo na ndipo Mahakama ilimtia hatiani na kumhukumu

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading