Ahadi ya TRA kwa mawakala wa forodha

Ahadi ya TRA kwa mawakala wa forodha

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Yusuph Mwenda, amewataka mawakala wa forodha nchini kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na kujiepusha na vitendo vya rushwa huku akiwaahidi mazingira bora ya kazi.

Ameyasema hayo jana Agosti 1, 2024, alipokutana na wanachama wa Chama cha Mawakala wa Forodha (TAFFA) kwa lengo la kusikiliza changamoto zao, kujadiliana namna ya kuzitatua na kuboresha huduma za forodha ili kuhakikisha wanalipa kodi stahiki.

Mwenda amesema wapo kwenye mchakato wa kuboresha mifumo yao ili kutimiza agizo la Rais Samia Suluhu Hassan ili kuweza kuingiza mapato mengi na kuondoa changamoto ya rushwa.

“Pale changamoto zitakapojitokeza naomba ushirikiano ili tufanye kazi pamoja kuepusha ucheleweshaji wa mizigo ya watu kukaa muda mrefu. Pia Serikali haitaki udanganyifu,” amesema.

“Neno rushwa linazungumzwa sana inaonekana rushwa zinatolewa sana. Nashauri hilo suala lisifanyike, ni kosa zaidi, tutaboresha ili huduma zitolewe haraka hasa kwenye maeneo ambayo kuna shida hiyo.”

Mwenda amewataka TAFFA wafanye kazi kwa kushirikiana na TRA ili kupunguza changamoto ya ucheleweshwaji wa mizigo huku akiwasisitiza kutopokea rushwa kutoka kwa wateja ili kuwahisha bidhaa zao.

Aidha, Mwenda amewahakikishia wanachama hao kuwa ameyachukua maoni yao na changamoto kwa yale yaliyokuwemo ndani ya uwezo wao watakwenda kuyafanyia kazi na yale ya kisera watayapeleka sehemu husika.

Kwa upande wake, Rais wa TAFFA, Edward Urio, amesema ushirikiano wao na maofisa wa idara ya forodha umewasaidia kuvuka malengo waliowekewa katika ukusanyaji kodi kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

“Tumevuka malengo ya ukusanyaji wa kodi kutokana na ushirikiano mzuri kati ya maofisa wa TRA na sisi mawakala wa forodha na kufanikiwa kukusanya kodi kwa niaba ya Serikali,” amesema Urio.

Amesema kwao ni faraja kubwa baada ya Mwenda kukubali kukutana nao na kujadiliana namna ya kuongeza ufanisi wa ukusanyaji kodi na kuboresha ushirikiano.

“Tunamuhakikishia kuwa malengo aliyopewa si yako pekee yake tutashirikiana naye kuhakikisha yanatimia,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading