Afrika yakabiliwa na uhaba wa marubani,wahandisi

Afrika yakabiliwa na uhaba wa marubani,wahandisi

Arusha. Ushindani katika usafiri wa anga katika Bara la Afrika unatajwa kuwa mdogo kutokana na mashirika ya ndege kuwa machache na kuwa yakiongezeka yatasaidia kuongeza ushindani,nauli kushuka pamoja na ubora wa huduma kuongezeka.

Aidha,  bara hilo linatajwa kuwa na upungufu wa rasilimali watu wakiwemo marubani na wahandisi katika sekta hiyo muhimu ambayo inazidi kukua kwa kasi.

Kutokana na sababu hizo,  wakurugenzi wakuu na wakuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Afrika ( AFCAC), wanakutana jijini Arusha kwa siku mbili kujadili namna ya kuboresha sekta hiyo.

Akizungumza katika mkutano huo leo Jumatano Juni 5, 2024, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa anga nchini (TCAA), Hamza Johari, amesema  malengo makubwa ni kuweka mikakati ya pamoja katika bara hilo kuhakikisha usafiri wa anga unakuwa salama.

“Tunataka tuangalie masuala ya kiushindani katika usafiri wa anga,tumeona kwamba ushindani si mkubwa sana kwani mashirika ya ndege ni machache,yanapokuwa machache nauli nazo zinakuwa juu tunataka yawe mengi,yanavyokuwa mengi yakashindana vizuri basi nauli na zenyewe zitarekebika.

” Tunataka tuangalie masuala ya rasilimali watu kwa maana ya kwamba tuna upungufu wa idadi ya marubani wanaohitajika katika sekta upungufu wa wahandisi wanaohitajika pia,”amesema Johari.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa Oktoba 5, 2023 mkurugenzi huyo, amesema kuanzia mwaka 2003 hadi 2023, idadi ya ndege zilizokuwa zinatoa huduma katika anga la Tanzania zimeongezeka kutoka 101 hadi 206,marubani wakitoka 234 hadi 603 huku waongoza ndege wakiongezeka kutoka 70 hadi kufikia 154.

Amesema kulikuwa na ongezeko la wakaguzi wa usalama kutoka 28 hadi 44, wahandisi wa mitambo ya viwanja wakiongezeka kutoka 20 hadi 44 na wataalam wa anga wakiongezeka kutoka 50 hadi kufika 83.

Kuhusu marubani amesema Tanzania inahitaji marubani 780 hivyo kuna upungufu mkubwa kuendana na kasi ya ukuaji ambapo hadi wakati huo walifadhili marubani 22 waliokuwa wakisoma nje ya nchi ila kwa sasa NIT itafundisha kwa Dola 48,000 ambazo ni sawa na Sh120.3 milioni badala ya Dola 120,000 zilizokiwa sawa na Sh300.9 milioni.

Hatua nyingine ni kuhakikisha usafiri wa anga Afrika unazidi kuwa salama na endelevu na kuwa wataangalia eneo la ulinzi kwani kumekuwa na tabia ya watu wenye nia ovu ikiwemo magaidi,kuteka ndege, kulipua viwanja na kutega mabomu japo matukio hayo hayatokei kwa wingi katika bara la Afrika lakini lazima wachukue tahadhari.

“Sasa hivi dunia imekua katika teknolojia kila kitu kinakwenda kidijitali na tunavyokwenda kwenye ulimwengu huo kunaweza kutokea mashambulio ya mifumo na mifumo ikiharibika tutashindwa kufanya shughuli zetu,tutaangalia zaidi uhalifu huo wa mitandaoni ili tusije kushambuliwa na tutengeneze sauti moja kama Afrika,”ameongeza Johari.

Akifungua mkutano huo, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema wakuu hao watajadiliana na kutoka na maazimio ya pamoja katika kuboresha usafiri huo pamoja na miundombinu huku suala la usalama likipewa kipaumbele kwani bila usalama hakuna usafiri wa anga wa uhakika.

Kuhusu suala la uchafuzi wa mazingira,Waziri Mbarawa amesema wakuu hao na wataalamu wa sekta ya anga watajadiliana jinsi wanaweza kuhakikisha anga linakuwa safi na salama na kuongeza maendeleo katika nchi hizo.

“Tanzania tumefanya kazi kubwa kwenye sekta ya usafiri wa anga na tuna miradi mbalimbali inaendelea na lengo la Serikali ni kuendelea kufungua usafiri wa anga na kuifanya anga zetu ziwe salama.

“Tunaendelea na ujenzi mkubwa wa viwanja vya ndege katika mikoa mbalimbali ikiwemo kiwanja cha Msalato Dodoma ambacho kitagharimu zaidi ya Sh365 bilioni,”amesema.

Waziri huyo amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha mikoa yote inakuwa na viwanja vya ndege vya kisasa na kuwataka Watanzania waendelee kutumia usafiri huo ambao ni usalama zaidi ukilinganisha na usafiri mwingine.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Karume faults lease of Zanzibar Islets
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Karume faults lease of Zanzibar Islets

Diplomat Ali Karume has faulted the decision by the revolutionary government of Zanzibar to lease the islets that surround the islands of Unguja and Pemba to private developers saying it was absolutely not in Zanzibar’s national interests.Continue Reading